Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 2:45 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

45 Uliliona jiwe lililoongoka lenyewe toka kwenye mulima, bila kuguswa, na jinsi lilivyoivunja vipandevipande ile sanamu iliyotengenezwa kwa chuma, shaba, udongo wa mufinyanzi, feza na zahabu. Ee mufalme, Mungu Mukubwa amekufunulia mambo yatakayotukia nyuma. Ni mimi ninayekuelezea hivyo. Ndoto yako ni ya kweli na maana yake ni ya kuaminiwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 2:45
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ngombe wale saba wazuri ni miaka saba, na yale masuke saba mazuri vilevile ni miaka saba. Ndoto hiyo tafsiri yake ni moja.


Kama vile nilivyokuelezea, ee mufalme, Mungu amekufunulia mambo atakayofanya sasa hivi.


Ndoto yako ilirudiliwa mara mbili kwa mifano inayofanana kwa kukuonyesha kwamba Mungu ameamua, naye atatimiza jambo hili sasa hivi.


Kutokana na yale tuliyosikia, wewe Yawe ni mukubwa. Hakuna anayekuwa kama wewe, na hakuna Mungu mwingine lakini wewe.


Maana Yawe ni mukubwa, anasifika sana anastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.


Ukiwa pahali popote unapofanya kazi, mara utakaposikia baragumu, kimbilia kwetu. Mungu wetu atatupigania.”


Kwa hiyo, ee Mungu wetu, Mungu mukubwa, mwenye nguvu na wa kutisha, wewe unashika agano lako na kutenda wema. Mateso yaliyotupata, sisi, wafalme wetu, wakubwa wetu, makuhani wetu, manabii wetu, babu zetu na watu wako wote tangu wakati wa wafalme wa Asuria mpaka leo, usiyaone kuwa ni madogo.


Mungu ni mukubwa sana hata hatuwezi kumujua; muda wa maisha yake hauchunguziki.


Ninajua hakika kwamba Yawe ni mukubwa; Bwana wetu ni mukubwa kupita miungu yote.


Yawe ni mukubwa, anastahili sifa nyingi; ukubwa wake hauwezi kuchunguzika.


Utawaponda kwa fimbo ya chuma, utawavunja kama chungu cha mufinyanzi!’ ”


Maana Yawe ni mukubwa, anasifiwa sana; anastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninaweka katika Sayuni jiwe la musingi, jiwe ambalo limeimarishwa. Jiwe la pembe, la bei kali, jiwe ambalo ni la musingi imara; jiwe linalokuwa na maandiko haya: Anayeamini hataanguka.


Basi, Danieli akamwendea Arioki aliyekuwa amechaguliwa kuwaangamiza wenye hekima wa Babeli, akamwambia: Usiwaue wenye hekima wa Babeli, lakini unipeleke mimi mbele ya mufalme, nami nitamweleza maana ya ndoto yake.


Lakini, kuna Mungu mbinguni ambaye anafumbua mafumbo, naye amekujulisha, ee mufalme Nebukadneza, mambo yatakayotukia katika siku zinazokuja. Ndoto yako na maono yaliyokufikia ulipokuwa unalala ni haya:


Ee mufalme, ulipokuwa unalala katika kitanda chako, mawazo yalikufikia juu ya mambo yatakayotukia kisha; naye Mungu anayefumbua mafumbo, alikuonyesha yale yatakayotukia.


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


Kwa werevu wake, atafanikiwa katika mipango yake ya udanganyifu, naye atajitukuza. Atawaangamiza watu wengi sana, na atataka kupigana na Mukubwa wa wakubwa, lakini ataangamizwa pasipo kutumia nguvu za kimutu.


na kuangusha falme na kukomesha nguvu zao. Nitayapindua magari yao ya vita na waaskari wapanda-farasi wake, nao wataanguka na kuuana wao kwa wao.


Siku hiyo nitaufanya Yerusalema kuwa kama jiwe zito kwa watu wote: yeyote atakayelinyanyua atajiumiza mwenyewe. Watu wa mataifa yote katika dunia wataushambulia muji ule.


Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.


Yesu akawajibu: “Nitawauliza ulizo moja tu. Kama mukinijibu, mimi vilevile nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.


Mbingu na dunia vitatoweka, lakini maneno yangu hayatabadilika hata kidogo.


Wafarisayo wakamwuliza Yesu: “Ufalme wa Mungu utakuja wakati gani?” Akawajibu: “Ufalme wa Mungu unakuja bila kutambulikana wazi.


Maana Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu wa miungu na Bwana wa wabwana. Yeye ni Mungu mukubwa na mwenye nguvu, na wa kuogopesha. Hapendelei wala hapokei kituliro.


Basi uandike mambo unayoona, na mambo yanayokuwa sasa na yale yatakayotokea nyuma.


Kisha nikaona malaika mumoja amesimama katika jua. Alikuwa akilalamikia ndege wote waliokuwa wakiruka juu katika anga akiwaambia: “Mukuje mukutane pamoja kwa karamu kubwa ya Mungu!


Nyuma ya mambo hayo nilipata maono mengine. Niliona mulango mumoja umefunguliwa wazi mbinguni. Halafu ile sauti niliyosikia mara ya kwanza, iliyolia kama baragumu, ikaniambia: “Panda huku, nami nitakuonyesha mambo yanayopaswa kutokea nyuma ya hayo ya mbele.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ