Danieli 2:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
34 Ulipokuwa ukiangalia, jiwe liliongoka lenyewe, bila kuguswa, na kuipondaponda miguu ya shaba na udongo wa mufinyanzi ya ile sanamu, na kuivunja vipandevipande.
Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninaweka katika Sayuni jiwe la musingi, jiwe ambalo limeimarishwa. Jiwe la pembe, la bei kali, jiwe ambalo ni la musingi imara; jiwe linalokuwa na maandiko haya: Anayeamini hataanguka.
Muungane, enyi watu wa mataifa, na kufezeheshwa! Musikilize, enyi inchi za mbali katika dunia! Mujiweke tayari na kufezeheshwa. Mujiweke tayari na kufezeheshwa.
Ufalme, utawala na ukubwa wa falme zote katika dunia watapewa kwa watu wa watakatifu wa Mungu Mukubwa. Ufalme wao utakuwa wa kudumu milele, na tawala zote zitawatumikia na kuwatii.
Kwa werevu wake, atafanikiwa katika mipango yake ya udanganyifu, naye atajitukuza. Atawaangamiza watu wengi sana, na atataka kupigana na Mukubwa wa wakubwa, lakini ataangamizwa pasipo kutumia nguvu za kimutu.
Siku hiyo nitaufanya Yerusalema kuwa kama jiwe zito kwa watu wote: yeyote atakayelinyanyua atajiumiza mwenyewe. Watu wa mataifa yote katika dunia wataushambulia muji ule.
Yule malaika akaniambia vilevile niseme neno hili la Yawe juu ya Zerubabeli: Hauwezi kushinda kwa nguvu au kwa uwezo wako mwenyewe, lakini kwa musaada wa roho wangu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema.
Kwa maana, tunajua kwamba hema hii tunayoishi ndani yake hapa katika dunia, maana yake mwili wetu, itakapobomolewa, Mungu atatupatia makao mengine mbinguni. Nayo ni nyumba aliyoijenga yeye mwenyewe na inayodumu milele.
Kwa maana Kristo hakuingia katika Pahali Patakatifu palipojengwa na watu, panapokuwa tu mufano wa Pahali Patakatifu kamili, lakini aliingia katika mbingu yenyewe, pahali anaposimama sasa mbele ya Mungu kwa kututetea.
Basi jiwe lile linahesabiwa kuwa la bei kali kwa wale wanaoamini. Lakini kwa wale wasioamini ni: “Jiwe lililotupiliwa na wajengaji, lakini sasa linakuwa jiwe kubwa la pembe.”
Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”
Watapigana vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo pamoja na waaminifu wake aliowaita na kujichagulia atawashinda, kwa sababu yeye ni Bwana wa wabwana na Mufalme wa wafalme.”