Yule mukubwa wa watumishi akawapa majina mengine; akamwita Danieli kwa jina la Beltesaza, Hanania kwa jina la Sadiraki, Misaeli kwa jina la Mesaki na Azaria kwa jina la Abedenego.
kwa sababu ana roho njema, maarifa, ujuzi wa kufasiria ndoto, kufumbua mafumbo na kutatua matatizo. Jina la mutu huyo ni Danieli ambaye baba yako alimwita Beltesaza. Basi wamwite, naye atakuelezea maana ya maandiko haya.
Lakini, nimesikia kwamba wewe unaweza kueleza vitendawili na kutambua mafumbo. Basi, kama ukiweza kusoma maandiko haya na kunielezea maana yake, utavalishwa nguo nzuri ya rangi nyekundu na kuvalishwa mukufu wa zahabu katika shingo lako. Utapewa nafasi ya tatu katika ufalme huu.
Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa mufalme Belsasari wa Babeli, Danieli aliota ndoto na kuona maono akiwa amelala katika kitanda chake. Akaandika ndoto yake hii: