Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 2:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Basi, Arioki akamupeleka Danieli mbele ya mufalme kwa haraka na kumwambia: Nimemupata mutu fulani kati ya wafungwa wa Yuda anayeweza kukufasiria maana ya ndoto yako, ee mufalme.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 2:25
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, mufalme akaamuru Yosefu aitwe; naye akaondolewa katika kifungo haraka. Kisha kunyoa na kubadilisha nguo zake, Yosefu akakuja mbele yake.


Wale waliokuwa katika uhamisho kule Babeli, walirudi Yerusalema na katika inchi ya Yuda, kila mumoja akarudi katika muji wake. Jamaa zao walikuwa wamekaa Babeli tangu mufalme Nebukadneza alipowahamishia kule wakiwa watumwa.


Umwokoe mutu anayepelekwa kuuawa kwa bure; usisite kumwopoa anayeuawa bila kosa.


Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.


Kati ya vijana waliochaguliwa kulikuwa Danieli, Hanania, Misaeli na Azaria, wote wa kabila la Yuda.


Basi, Danieli akaletwa mbele ya mufalme, naye mufalme akamwuliza: Wewe ndiwe Danieli, mumoja wa wafungwa ambao baba yangu mufalme, aliowaleta kutoka inchi ya Yuda?


Basi, walikwenda kwa mufalme na kumushitaki Danieli kwa kutumia ile sheria, wakisema: Mufalme Dario, haukutia sahihi kwenye sheria kwamba kwa muda wa siku makumi tatu hakuna mutu yeyote atakayeruhusiwa kuomba kitu chochote, kwa mungu yeyote, au kwa mutu yeyote isipokuwa kutoka kwako wewe, ee mufalme, na kwamba yeyote atakayevunja sheria hii atatumbukizwa katika pango la simba? Mufalme akaitikia: Hivi ndivyo inavyokuwa kulingana na sheria ya Wamedi na Wapersi ambayo haiwezi kuvunjika.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ