Majani yake yalikuwa mazuri. Ulikuwa umejaa matunda mengi yaliyotoshelea kwa kulisha dunia nzima. Nyama wote wa pori walipata kivuli chini yake, na ndege wa anga walikaa katika matawi yake. Viumbe vyote vilipata chakula kutoka muti huo.
Kisha, katika maono hayo yangu ya usiku, nikaona nyama wa ine wa ajabu na wa kutisha, mwenye nguvu sana. Huyu alikuwa na meno makubwa ya chuma ambayo aliyatumia kwa kula na kuvunjavunja, na mabaki aliyakanyagakanyaga. Alikuwa tofauti na wale nyama wengine watatu, maana alikuwa na pembe kumi.
Habari hiyo ikawafurahisha Waisraeli, wakamushukuru Yawe na kuacha mipango yao ya vita na kusudi lao la kuharibu kabisa inchi iliyokuwa ya makabila ya Rubeni na Gadi.