Mungu anasema: Kisha kutaabika sana, mutumishi wangu atafurahi. Kwa njia ya kujulikana kwa huyo mutumishi wangu wa haki, atawafanya wengi wakuwe wenye haki, naye atazibeba zambi zao.
Kama wangalihuzuria katika baraza langu, wangalitangazia watu wangu maneno yangu, wangaliwageuza kutoka katika njia zao mbaya, na kutoka katika matendo yao maovu.
Wenye hekima kati ya watu watawafundisha wengi. Hata hivyo, kwa siku chache watauawa kwa upanga au kwa moto, watakamatwa mateka au kunyanganywa mali zao.
Watu wengi wataondolewa uchafu, watatakaswa na kusafishwa. Lakini watu waovu wataendelea kutenda uovu. Hakuna hata mumoja wa hao waovu atakayeelewa; wenye hekima ndio watakaoelewa.
Yesu akawajibu: “Kweli ninawaambia: Katika ulimwengu mupya, Mwana wa Mutu atakapoikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu, ninyi kumi na wawili mulionifuata mutaikaa vilevile juu ya viti kumi na viwili vya kifalme kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.
“Basi ni nani anayekuwa mutumishi mwaminifu na mwenye akili? Ni yule bwana wake aliyemuweka kuwa musimamizi wa watumishi wake wengine na kumwamuru kuwapatia posho yao kwa wakati uliopangwa.
Katika kanisa la Antiokia kulikuwa manabii na walimu wamoja. Kati yao kulikuwa Barnaba, Simoni aliyeitwa vilevile Nigeri; Lukio wa Kurene, Saulo na Manaeni, aliyekomaa pamoja na mufalme Herode.
Kwa kadiri ya zawadi Mungu aliyonipatia, kama vile fundi wa kujenga mwenye hekima, niliweka musingi. Na sasa, mutu mwingine anajenga juu yake. Lakini inafaa kila mutu aangalie vizuri namna anavyojenga.
Ni yeye ndiye aliwapatia watu zawadi za kipekee. Amewaweka wamoja kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa watangazaji wa Habari Njema, wengine kuwa wachungaji na walimu.
Kweli, kwa wakati huu, ninyi mungepaswa sasa kuwa walimu, lakini mungali munahitaji kufundishwa tena mafundisho ya mwanzo ya neno la Mungu. Mumegeuka tena wenye kuhitaji kunywa maziwa, wala si chakula kigumu.
Mutambue kwamba njia ya kuvumilia kwa Bwana wetu ni wakati muzuri anaowapatia kusudi mupate kuokolewa. Na hiyo ni kufuatana na vile ndugu yetu mupendwa Paulo alivyowaandikia akiongozwa na hekima aliyopewa na Mungu.
Hii ndiyo maana ya lile fumbo juu ya zile nyota saba ulizoona katika mukono wangu wa kuume, na vile vinara saba vya zahabu: zile nyota saba ni wamalaika wa makanisa saba na vile vinara saba ni yale makanisa saba.
“Ee Yawe, waangamie waadui zako wote! Lakini warafiki zako wakuwe kama jua, wakati linapochomoza kwa mwangaza mukubwa!” Inchi ya Waisraeli ikakuwa na amani kwa muda wa miaka makumi ine.