Danieli 12:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20021 Wakati huo, Mikaeli, malaika mukubwa, anayekuwa mulinzi wa watu wako, atatokea. Halafu kutakuwa wakati wa taabu sana kuliko nyakati zingine zote tangu mataifa yalipoanza kuwa katika dunia. Lakini, wakati huo, kila mumoja wa watu wako ambaye jina lake limeandikwa katika kitabu cha uzima, ataokolewa. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Nitanyoosha mukono wangu juu yenu ninyi manabii munaotoa maono ya uongo na kutabiri udanganyifu mutupu. Watu wangu watakapokutanika kwa kuamua maneno, ninyi hamutakuwa pale. Wala hamutakuwa katika kitabu cha majina ya Waisraeli na hamutaingia katika inchi ya Waisraeli; halafu mutatambua kwamba mimi ni Bwana wenu Yawe.