Danieli 11:37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
37 Mufalme huyo hataijali miungu ya babu zake wala yule anayependwa na wanawake. Ataizarau miungu mingine yote, maana atajiweka kuwa mukubwa kuliko kila mumoja wao.
Wewe ulijisemesha ndani ya moyo wako: Nitapanda mpaka mbinguni; nitaweka kiti changu juu ya nyota za Mungu, nitaikaa juu ya mulima pahali miungu wanapokutana, huko mbali pande za kaskazini.
Wewe mwanadamu! Umwambie mufalme wa Tiro kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wewe una kiburi cha moyo, na umesema kwamba wewe ni mungu, kwamba umeikalia kiti cha kifalme cha miungu, umekaa mbali huko katika bahari. Lakini, wewe ni mutu tu wala si mungu, ingawa unajiona kuwa na hekima kama mungu.
Mufalme atafanya kama anavyopenda. Atajitukuza na kujivuna kwamba yeye ni mukubwa kuliko miungu yote, na kumutukana Mungu wa miungu. Ataendelea kufanikiwa mpaka kasirani ifikie ukomo wake, maana yaliyopangwa sherti yatimie.
Pahali pa miungu hiyo atamuheshimu mungu mulinzi wa kuta za muji, ambaye babu zake hawakumwabudu hata kidogo. Atamutolea zahabu, feza na mawe ya bei kali, na zawadi za bei kubwa.
Pembe dogo ile ikajitukuza mbele ya mukubwa wa viumbe vya mbinguni. Ikakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto ambazo mukubwa wa viumbe vya mbinguni alivyotambikiwa kila siku, na kuchafua hekalu lake.
“Usimutamani muke wa mwenzako, wala nyumba yake, wala shamba lake, wala mutumwa wake au mujakazi wake, wala ngombe wake, wala punda wake, wala kitu chochote mwenzako anachokuwa nacho.”
Yeye atapinga kitu chochote watu wanachohesabu kuwa cha kimungu au wanachoabudu na kujiweka kuwa juu ya vyote. Yeye ataenda hata kuingia katika hekalu la Mungu na kukaa mule na kujiita mwenyewe kuwa Mungu.
Wao wanafundisha kwamba ni vibaya kuoana, na wanawakataza watu kula vyakula fulani fulani. Lakini Mungu aliumba vyakula vile kusudi watu waliokwisha kumwamini na kutambua ukweli wapate kuvitumia wakisha kumushukuru.