Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 11:36 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

36 Mufalme atafanya kama anavyopenda. Atajitukuza na kujivuna kwamba yeye ni mukubwa kuliko miungu yote, na kumutukana Mungu wa miungu. Ataendelea kufanikiwa mpaka kasirani ifikie ukomo wake, maana yaliyopangwa sherti yatimie.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 11:36
47 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mumushukuru Mungu wa miungu. Wema wake unadumu milele.


Yawe anavunja mipango ya mataifa, na anabadilisha mawazo yao.


Katika moyo wa mutu muna mipango mingi, lakini anachokusudia Yawe ndicho kitakachokamilika.


Kweli! Bwana, Yawe wa majeshi, atakamilisha kabisa katika inchi yote jambo aliloamua kutenda.


Maana bado kidogo, nayo hasira yangu itapita na kasirani yangu itawageukia Waasuria.


Ole kwake Asuria, yeye ni kama fimbo ya hasira yangu, yeye anayeshika kiboko cha hasira yangu!


Wewe ulijisemesha ndani ya moyo wako: Nitapanda mpaka mbinguni; nitaweka kiti changu juu ya nyota za Mungu, nitaikaa juu ya mulima pahali miungu wanapokutana, huko mbali pande za kaskazini.


Nitapanda juu ya mawingu nitajifanya kuwa sawa na Mungu Mukubwa.


Mukuje watu wangu, muingie ndani ya nyumba zenu, mujifungie humo ndani. Mujifiche kwa muda mufupi, mpaka kasirani ya Yawe ipite.


Kweli, pahali pa kumuteketeza mufalme wa Asuria pamekwisha kutayarishwa muda murefu uliopita. Pahali penyewe ni shimo kubwa na pana. Kuna moto na kuni kwa uwingi. Yawe ataupulizia pumzi yake kama kijito cha kiberiti na kuuwasha.


Nilitangaza mambo ya mwisho tangu mwanzo, tangu zamani nilitangaza mambo yatakayotukia. Kusudio langu litatimia; mimi nitatimiza nia yangu yote.


Munajipakaa marasi na mafuta kwa wingi kisha munakwenda kumwabudu Moleki. Munawatuma wajumbe wenu huko na huko, kujitafutia miungu ya kuabudu; hata kuzimu walifika.


Wewe mwanadamu! Umwambie mufalme wa Tiro kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wewe una kiburi cha moyo, na umesema kwamba wewe ni mungu, kwamba umeikalia kiti cha kifalme cha miungu, umekaa mbali huko katika bahari. Lakini, wewe ni mutu tu wala si mungu, ingawa unajiona kuwa na hekima kama mungu.


Nimesikia jinsi unavyojivuna na kusema maneno mengi juu yangu.


Mushambulizi atawatendea sawa anavyopenda; hakuna atakeyesubutu kupingana naye. Atasimama katika inchi tukufu, na inchi hiyo yote itakuwa chini ya mamlaka yake.


Kisha kutatokea mufalme hodari atakayetawala eneo kubwa na kufanya atakavyopenda.


Mufalme huyo hataijali miungu ya babu zake wala yule anayependwa na wanawake. Ataizarau miungu mingine yote, maana atajiweka kuwa mukubwa kuliko kila mumoja wao.


Yule mutu aliyesimama upande wa juu wa muto, aliyevaa nguo za kitani, akainua mikono yake yote miwili kuelekea mbinguni. Kisha nikamusikia akiapa kwa jina la yule anayeishi milele: Itakuwa muda wa nyakati tatu na nusu. Wakati mateso ya watu watakatifu yatakapokomeshwa, mambo haya yote yatakuwa yametimia.


Mufalme akamwambia Danieli: Hakika, Mungu wako ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme, na ndiye anayefumbua mafumbo kwa sababu ameweza kunifumbulia fumbo hili.


Kwa sababu ya ukubwa aliomupa, watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote walitetemeka na kumwogopa. Nebukadneza aliweza kumwua mutu yeyote aliyetaka na kumwacha muzima mutu yeyote aliyetaka. Aliyetaka kumupandisha cheo alimupandisha, aliyetaka kumushusha cheo alimushusha.


Lakini alipoanza kuwa na kiburi, akakuwa na roho ngumu na mwenye majivuno, aliondolewa katika kiti chake cha kifalme, akanyanganywa utukufu wake.


Nilipokuwa ninaziangalia hizo pembe, niliona pembe ingine ndogo ikiota katikati ya zile kumi, nayo ikaongoa pembe tatu kati ya hizo za kwanza. Pembe ile ilikuwa na macho ya kimutu na kinywa kilichosema maneno ya kujivuna.


Kisha akaniambia: Sikiliza, ninakufahamisha jinsi matokeo ya kasirani ya Mungu yatakavyokuwa. Maono hayo yanaelekea wakati wa mwisho.


Nilimwona huyo kondoo dume akishambulia kuelekea upande wa magaribi, kaskazini na kusini. Hakuna nyama yeyote aliyesubutu kusimama mbele yake, wala kuziepuka nguvu zake. Alifanya sawa anavyopenda na kujitukuza mwenyewe.


Maana nitaleta katika inchi muchungaji asiyemujali kondoo anayeangamia, au kumutafuta kondoo anayetangatanga, au kumutunza aliyeumizwa wala kumukulisha yule anayekuwa muzima: lakini atakula wale kondoo wanono, hata kwato zao.


“Siwezi kufanya kitu kwa mafikiri yangu mwenyewe. Ninahukumu tu kama vile Mungu anavyoniambia na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu sitafuti kufanya mapenzi yangu, lakini mapenzi ya yule aliyenituma.


Kwa sababu nimeshuka toka mbinguni kusudi nifanye mapenzi ya yule aliyenituma, wala si mapenzi yangu.


Hivi walitimiza mambo uliyokuwa umekusudia tangu zamani kwa uwezo wako na kwa mapenzi yako.


Maana Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu wa miungu na Bwana wa wabwana. Yeye ni Mungu mukubwa na mwenye nguvu, na wa kuogopesha. Hapendelei wala hapokei kituliro.


Musikubali kudanganywa na mutu yeyote kwa namna yoyote. Kwa maana Siku ile haitatimia mpaka kwanza ule uasi mukubwa utokee na yule Mwovu aonekane ambaye mwisho wake ni kuangamizwa.


Yeye atapinga kitu chochote watu wanachohesabu kuwa cha kimungu au wanachoabudu na kujiweka kuwa juu ya vyote. Yeye ataenda hata kuingia katika hekalu la Mungu na kukaa mule na kujiita mwenyewe kuwa Mungu.


Halafu, yule Mwovu atatokea, lakini Bwana Yesu atakapotokea atamwua kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kwa nguvu za kumetameta kwake.


“Mungu wa miungu ndiye Yawe! Mungu wa miungu ndiye Yawe! Yeye anajua kwa nini tumefanya hivyo. Na Waisraeli wote watajua vilevile! Kama huu ni uasi au ni ukosefu wa imani kwa Yawe basi, yeye aache kutuokoa leo.


Lakini wakati malaika wa saba atakapopiga baragumu, Mungu atatimiza mipango yake aliyoficha sawa vile alivyotangaza kwa kinywa cha manabii waliomutumikia.


Lakini yule mwanamuke akapewa mabawa mawili yanayokuwa kama ya tai, kusudi apate kuruka kwenda katika jangwa kwenye nafasi aliyotengenezewa, mbali na yule nyoka. Na kule apate kukulishwa kwa muda wa miaka mitatu na nusu.


Kisha nikaona nyama mumoja wa ajabu akitokea ndani ya bahari. Alikuwa na vichwa saba na pembe kumi. Na juu ya kila pembe lake kulikuwa taji, na juu ya vichwa vile kulikuwa kumeandikwa jina la kumutukana Mungu.


Kwa maana Mungu ametia ndani yao nia ya kuwasukuma kutimiza shabaha yake nao wapate kufikia shauri moja na kumupa yule nyama madaraka yao ya kifalme mpaka maneno ya Mungu yatimie.


Nikashikwa na Roho wa Mungu, na malaika akanipeleka katika jangwa. Kule nikaona mwanamuke aliyekuwa akiikaa juu ya nyama mumoja wa ajabu mwekundu aliyeandikwa juu yake majina ya kumutukana Mungu. Nyama yule alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ