Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 11:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Katika wakati uliopangwa ataishambulia inchi ya kusini kwa mara ingine, lakini mara hii, mambo yatakuwa tofauti.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 11:29
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ulie ewe mulango; ulalamike ewe muji; tetemeka kwa hofu, ewe inchi yote ya Filistia. Maana moshi wa waaskari unakuja kutoka kaskazini, wala hakuna atakayechelewa katika makundi yake.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Kiro wa Persia, Danieli, aliyeitwa vilevile Beltesaza, alipewa ufunuo. Ufunuo huo ulikuwa wa kweli, lakini ulikuwa mugumu sana. Hata hivyo alielewa ufunuo huo maana alifahamu maono vilevile.


Kwa kufanya mapatano, atayadanganya mataifa mengine, na ataendelea kupata nguvu ingawa atatawala taifa dogo.


Kwa uhodari mwingi, ataunda kundi kubwa la waaskari kusudi apate kuushambulia ufalme wa kusini, naye mufalme wa kusini atajibu mashambulizi hayo kwa kundi kubwa zaidi la waaskari na lenye nguvu sana. Lakini, mufalme wa kusini hatashinda kwa maana watafanya shauri baya juu yake.


Mufalme wa kaskazini atarudi katika inchi yake akiwa na mali nyingi, lakini nia yake ndani ya moyo ni kulivunja agano takatifu. Atafanya vile anavyopenda, kisha atarudi katika inchi yake.


Mashua kutoka Kitimu zitamushambulia, naye atashikwa na hofu. Kisha atarudi nyuma akiwa amejaa hasira na kuvunja agano takatifu. Halafu atafuata shauri la wale walioasi agano takatifu.


Kisha akaniambia: Sikiliza, ninakufahamisha jinsi matokeo ya kasirani ya Mungu yatakavyokuwa. Maono hayo yanaelekea wakati wa mwisho.


Kutokana na mutu mumoja, yeye aliumba watu wa mataifa yote kusudi waishi katika dunia yote. Aliwapangia nyakati na kukata mipaka ya inchi wanayopaswa kukaa ndani yake.


Kwa muda ule yeye ni chini ya madaraka ya watu wanaomuchunga na ya walinzi wa mali mpaka wakati baba yake aliopanga upate kutimia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ