Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 11:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Sasa nitakuelezea ule ukweli wa mambo haya. Wafalme wengine watatu wataitawala inchi ya Persia. Hao watafuatwa na mufalme wa ine ambaye atakuwa tajiri kuliko wale waliomutangulia. Wakati atakapopata nguvu kwa ajili ya utajiri wake, ataanza kuushambulia ufalme wa Ugriki.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 11:2
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kazi ya kuijenga upya nyumba ya Mungu katika Yerusalema ilisimama, na hali hiyo ikaendelea mpaka mwaka wa pili wa utawala wa Dario, mufalme wa Persia.


Tena wakati wa utawala wa Artasasta, mufalme wa Persia, Bisilamu, Mitiredati, Tabeli na warafiki zao, wakamwandikia barua mufalme Artasasta. Barua hiyo iliandikwa katika herufi za Kiaramea na kutafsiriwa.


Mufalme Ahasuero alipotawala ufalme wake ulikuwa na majimbo mia moja makumi mbili na saba, toka Uhindi mpaka Etiopia.


kwa kukufundisha mambo yanayokuwa sawa na kweli; na mutu akikuuliza upate kumupa jibu la kweli.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Kiro wa Persia, Danieli, aliyeitwa vilevile Beltesaza, alipewa ufunuo. Ufunuo huo ulikuwa wa kweli, lakini ulikuwa mugumu sana. Hata hivyo alielewa ufunuo huo maana alifahamu maono vilevile.


Kwa uhodari mwingi, ataunda kundi kubwa la waaskari kusudi apate kuushambulia ufalme wa kusini, naye mufalme wa kusini atajibu mashambulizi hayo kwa kundi kubwa zaidi la waaskari na lenye nguvu sana. Lakini, mufalme wa kusini hatashinda kwa maana watafanya shauri baya juu yake.


Nyama wa pili alikuwa kama dubu ambaye upande wake mumoja ulikuwa umeinuka. Na katika kinywa chake alikuwa na mifupa mitatu ya mbavu aliyoishika kwa meno yake. Sauti ikamwambia: Simama, ukule nyama nyingi kadiri unavyoweza.


Yule beberu ni mufalme wa Ugriki. Ile pembe kubwa katikati ya macho yake ni mufalme wa kwanza.


Maono ya hizo nyakati za magaribi na za asubui ambayo yameelezwa ni ya kweli. Lakini uyafiche, sababu ni siri, maana yatatokea kisha siku nyingi.


Nilimwona huyo kondoo dume akishambulia kuelekea upande wa magaribi, kaskazini na kusini. Hakuna nyama yeyote aliyesubutu kusimama mbele yake, wala kuziepuka nguvu zake. Alifanya sawa anavyopenda na kujitukuza mwenyewe.


Hakika, Bwana wetu Yawe hafanyi kitu bila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake.


Maandiko Matakatifu hayawezi kuvunjwa. Mungu aliwaita ‘miungu’ wale walioambiwa neno lake.


Basi yule aliyekuwa akiikaa juu ya kiti cha kifalme akasema: “Angalia ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Kisha akaniambia: “Andika maneno haya, kwa maana ni ya kweli na ya uhakika.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ