19 Halafu atageuka kurudi katika kuta za inchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka katika vita na huo ndio utakaokuwa mwisho wake.
Atatoweka kama ndoto, asionekane tena, atafutikana kama maono ya usiku.
Anawaangamiza wenye nguvu bila uchunguzi, na kuwaweka wengine pahali pao.
Waovu wakinishambulia, na kutaka kuniangamiza, hao wapinzani wangu watajikwaa na kuanguka.
Nilimwona mwovu aliyejivuna sana, akinyanyua shingo juu kama mierezi ya Lebanoni!
Kisha nikapita pale, naye hakukuwa tena; nikamutafuta, lakini hakuonekana tena.
Inapepesuka kama mulevi, inayumbayumba kama kibanda. Imelemewa na muzigo wa zambi zake nayo itaanguka wala haitasimama tena.
Wanaokuwa wepesi hawawezi kutoroka, mashujaa hawawezi kukwepa; huko kaskazini kwenye muto Furati wamejikwaa na kuanguka.
Nitakufanya kuwa kitu cha kuogopesha na itakuwa mwisho wako; watu watakutafuta, lakini hawatakupata tena. –Ni Bwana wetu Yawe anayesema hivyo.
Kisha mutoto mumoja wa ukoo wa huyo binti atakuwa mufalme. Huyo atayashambulia makundi ya waaskari wa mufalme wa kaskazini na kuingia katika miji yao yenye kuzungukwa na kuta na kushinda.