Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 11:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Halafu mufalme wa kaskazini atalundika udongo kando ya muji wenye kuta imara na kuuteka. Waaskari wa kusini hawataweza kuupiganisha, hata wale wafundi wa vita, maana hawatakuwa na nguvu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 11:15
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maana Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi juu ya nyumba za Yerusalema na nyumba za wafalme wa Yuda zilizobomolewa kwa sababu ya vita.


Mupande, mupite katika mashamba yake ya mizabibu, muharibu kila kitu lakini musivimalize kabisa. Mukate matawi yake, kwa maana hayo si yangu mimi Yawe.


Ikakuwa katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, mwaka wa kenda wa utawala wa Zedekia, Nebukadneza mufalme wa Babeli, alifika na waaskari wake wote kuushambulia Yerusalema, wakauzunguka kila upande.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mukate miti na kulundika udongo, kwa kuweza kupandia ndani ya Yerusalema. Muji huu unapaswa uazibiwe, maana hamuna lolote ndani yake isipokuwa ukorofi tu.


Hakika, Mufalme wa Misri pamoja na jeshi lake kubwa hataweza kumusaidia katika vita wakati Wababeli watakapomuzungushia kikingio na kuta kusudi wapate kuwaua watu wengi.


Onyesha kwamba muji ule umeshambuliwa. Utaujengea nafasi za kupandia juu ya kuta zake. Kandokando yake uweke makambi ya waaskari, na gongo ya kubomoa kuta.


Wakati huo watu wengi watamwasi mufalme wa kusini. Watu wamoja waovu wa taifa lako wewe Danieli, wataasi kwa kutimiza maono haya, lakini watashindwa.


Kisha miaka michache, wataungana pamoja; binti wa mufalme wa kusini ataolewa katika jamaa ya mufalme wa kaskazini na kutimiza mapatano hayo, lakini hataendelea kuwa na nguvu, hata mufalme na wazao wake hawatavumilia; na huyo binti, mwana wake na wajakazi aliokwenda nao, wote watauawa.


Nilimwona akimusogelea yule kondoo dume. Alikuwa amemukasirikia sana yule kondoo dume, hivyo akamushambulia kwa nguvu na kuzivunja zile pembe zake mbili. Yule kondoo dume hakuweza kuvumilia. Aliangushwa chini na kukanyagwakanyagwa, wala hakuna yeyote kwa kumwokoa toka katika nguvu zake.


Hakuna mutu atakayekushinda siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Musa. Siku zote nitakuwa nawe wala sitakuacha hata kidogo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ