Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 10:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Lakini nitakujulisha yale yaliyoandikwa katika kitabu cha ukweli. Sina mwingine wa kunisaidia kwa kuwashinda hawa isipokuwa Mikaeli, malaika mulinzi wenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 10:21
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mukubwa wa ufalme wa Persia alinipinga kwa muda wa siku makumi mbili na moja. Lakini Mikaeli, mumoja kati ya wakubwa, akakuja kunisaidia, kwa hiyo nikamwacha kule pamoja na mukubwa wa ufalme wa Persia,


Wakati huo, Mikaeli, malaika mukubwa, anayekuwa mulinzi wa watu wako, atatokea. Halafu kutakuwa wakati wa taabu sana kuliko nyakati zingine zote tangu mataifa yalipoanza kuwa katika dunia. Lakini, wakati huo, kila mumoja wa watu wako ambaye jina lake limeandikwa katika kitabu cha uzima, ataokolewa.


Lakini sasa, Danieli, weka kwa siri mambo hayo; funga kitabu na kutia muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho utakapofika. Wengi watakimbilia huko na huko, na maarifa yataongezeka.


Maono ya hizo nyakati za magaribi na za asubui ambayo yameelezwa ni ya kweli. Lakini uyafiche, sababu ni siri, maana yatatokea kisha siku nyingi.


Basi, akaniambia: Danieli, nimekuja kukupa hekima na uwezo wa kufahamu.


Basi, ujue na kufahamu jambo hili: tangu wakati amri itakapotolewa ya kujengwa upya Yerusalema mpaka kuja kwa yule aliyepakwa mafuta, yule anayekuwa mukubwa, ni muda wa majuma saba. Kwa muda wa majuma makumi saba na mawili, Yerusalema utajengwa upya, wenye barabara kubwa na kuta, lakini wakati huo utakuwa wa taabu.


Hakika, Bwana wetu Yawe hafanyi kitu bila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake.


Na jambo hilo linapatana na maneno haya ya manabii yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu:


Ni vile Bwana anavyosema, yeye aliyejulisha mambo haya tangu zamani za kale.’ ”


Hata Mikaeli, malaika mukubwa, aliposhindana na kubishana na Shetani juu ya maiti ya Musa, hakusubutu kumuhukumu kwa matusi, lakini alisema: “Bwana mwenyewe akukaripie.”


Halafu kukatokea vita katika mbingu. Mikaeli na wamalaika zake wakapigana na yule nyoka mukubwa. Naye yule nyoka akapigana nao pamoja na wamalaika zake,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ