15 Alipokuwa ananiambia maneno hayo, niliangalia chini bila kuweza kusema.
Siku hiyohiyo, utaacha kuwa bubu, nawe utaweza kuongea naye. Kwa hiyo wewe utakuwa kitambulisho kwao, nao watatambua kwamba mimi ni Yawe.
Nitaufanya ulimi wako ukuwe muzito nawe utakuwa bubu kusudi usiweze kuwakaripia kwa sababu ni waasi.
Wakati mutu huyo alipofika, ilikuwa asubui. Jana yake magaribi Yawe alikuwa amenijaza uwezo wake nami sikuwa bubu tena, nikaanza kusema.
Nilipoisikia sauti yake, nilianguka uso mpaka chini, nikashikwa na usingizi muzito.
Alipokuwa anazungumuza nami, mimi nikashikwa na usingizi muzito nikiwa nimelala uso mpaka chini. Lakini yeye akanishika na kunisimamisha.
Maneno yale yatatimia kwa wakati wake uliopangwa, lakini kwa sababu haukuyasadiki, utakuwa bubu. Hautaweza kusema mpaka siku ile mambo hayo yatakapotimia.”