Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Danieli 10:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 nami nimekuja kukusaidia upate kuyafahamu mambo yatakayowapata watu wako wakati unaokuja, maana maono uliyoona yanaelekea wakati unaokuja.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Danieli 10:14
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yakobo akawaita wana wake, akasema: “Mukusanyike pamoja niwaambie mambo yatakayowapata siku zinazokuja.


Katika siku zinazokuja, itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe utaimarishwa kupita milima yote, utainuliwa juu ya vilima vyote. Mataifa yote yatajaa kule,


Wewe mwanadamu, Waisraeli wanafikiri kwamba maono yako yanahusu siku za nyuma sana, na unabii wako unahusu nyakati za mbali sana!


Utawashambulia Waisraeli, kama vile wingu linalotanda juu ya inchi. Wakati huo nitakutuma uishambulie inchi yangu, kusudi mataifa yajue kwamba nimekutumia wewe Gogi kusudi nionyeshe utakatifu wangu mbele yao.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Kiro wa Persia, Danieli, aliyeitwa vilevile Beltesaza, alipewa ufunuo. Ufunuo huo ulikuwa wa kweli, lakini ulikuwa mugumu sana. Hata hivyo alielewa ufunuo huo maana alifahamu maono vilevile.


Lakini sasa, Danieli, weka kwa siri mambo hayo; funga kitabu na kutia muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho utakapofika. Wengi watakimbilia huko na huko, na maarifa yataongezeka.


Akanijibu: Danieli, ujiendee, maana maneno haya ni siri na yamefungwa kwa kutiwa muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho.


Lakini, kuna Mungu mbinguni ambaye anafumbua mafumbo, naye amekujulisha, ee mufalme Nebukadneza, mambo yatakayotukia katika siku zinazokuja. Ndoto yako na maono yaliyokufikia ulipokuwa unalala ni haya:


Nikasikia sauti ya mwanadamu kutoka katika muto Ulayi ikiita: Gabrieli, umwelezee mutu huyu maana ya maono aliyoona.


Maono ya hizo nyakati za magaribi na za asubui ambayo yameelezwa ni ya kweli. Lakini uyafiche, sababu ni siri, maana yatatokea kisha siku nyingi.


Basi, akaniambia: Danieli, nimekuja kukupa hekima na uwezo wa kufahamu.


Nyuma, Waisraeli watarudi na kumutafuta Yawe, Mungu wao, na kumutafuta mufalme wao, wa uzao wa Daudi. Halafu watamutii Yawe, na kutazamia wema wake siku za mwisho.


Kutakuja wakati ambapo mulima wa nyumba ya Yawe utakuwa mukubwa kuliko milima yote. Utanyanyuliwa juu ya vilima vyote. Watu wengi watakimbilia kule,


Maono haya yanangoja wakati uliopangwa; ni maono ya ukweli juu ya mwisho. Kama yanaonekana kuchelewa, uyangojee; hakika yatafika, wala hayatachelewa.


Sasa ninarudi kwa watu wangu, lakini mbele sijaondoka, acha nikuambie mambo ambayo watu hao watawatendea watu wako siku zinazokuja.


Watakapopatwa na hasara nyingi na taabu, wimbo huu utakuwa kama ushuhuda maana hautasahauliwa na wazao wao. Hata sasa, mbele sijawapeleka katika inchi niliyoapa kuwapa, ninajua mipango ambayo wanapanga.”


Maana ninajua kwamba nyuma ya kifo changu hakika mutakuwa waovu na kuacha ile njia niliyowaamuru muifuate. Na katika siku zinazokuja mutapatwa na hasara kwa sababu mutafanya maovu mbele ya Yawe na kumukasirikisha kwa matendo yenu.”


Mambo haya yote yatakapowapata huko, kisha mukipata taabu, mutamurudilia Yawe na kumutii.


Ujue vizuri kwamba siku za mwisho zitakuwa nyakati za magumu.


Basi, namna gani sisi tutaponyoka azabu kama hatushuguliki na wokovu mukubwa kama huu? Ni Bwana mwenyewe aliyetangaza kwanza habari za wokovu huu, na wale waliomusikia walihakikisha kwetu kwamba ni za kweli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ