Mulimaji anapopepeta ngano yake, haendelei kuipepeta mpaka kuvunja punje zake. Anajua jinsi ya kuipepeta kwa gurudumu la gari, bila kuharibu punje za ngano.
Pumzi yake ni kama mafuriko ya muto ambao maji yake yanafika mpaka kwenye shingo. Anakuja kupepeta mataifa kwa lungo ya maangamizi, kuwafunga lijamu na kuwapeleka wasikotaka.
Ikiwa itanifikia kuvunja mipango ile, halafu nitaweza vilevile kukomesha kizazi cha Waisraeli, wasiitwe tena taifa langu siku zote. –Ni ujumbe wa Yawe.
Usiogope, ee Yakobo mutumishi wangu, kwa maana mimi niko pamoja nawe. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambayo nimekutawanya kati yao, lakini wewe sitakuangamiza. Nitakuazibu kadiri unavyostahili, sitakuacha bila kukuazibu.
Nitaondoa kati yenu waasi na wale wanaonikosea; nitawaondoa katika inchi walikokaa kama wakimbizi, lakini hawataingia hata kidogo katika inchi ya Waisraeli. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.
Kisha watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wao, kwa sababu mimi niliwapeleka katika uhamisho kati ya mataifa na kuwarudisha tena katika inchi yao. Sitamwacha hata mutu wao mumoja abakie kati ya mataifa.
Hukohuko katika muji wazazi watawakula watoto wao wenyewe na watoto watawakula wazazi wao. Nitatimiza hukumu zangu juu yenu na watakaobaki wazima nitawasambaza pande zote.
Sehemu moja ya tatu ya watu wako, ee Yerusalema, itakufa kwa ugonjwa mukali na kwa njaa. Sehemu ingine moja ya tatu itakufa katika vita. Na sehemu moja ya tatu inayobaki nitaisambaza pande zote za dunia na nitachomoa upanga wangu na kuwafuatilia nyuma.
Yawe atawatawanya kati ya mataifa yote, kutoka pembe moja ya dunia mpaka nyingine na huko mutaitumikia miungu mingine ya miti na mawe, miungu ambayo ninyi wala wazee wenu hamukuijua.