Hivyo akasema: “Nitamuharibu kabisa katika dunia mwanadamu niliyemwumba, pamoja na nyama wa pori, viumbe vinavyotambaa na ndege wa anga. Ninasikitika kwamba niliwaumba katika dunia.”
Nyuma ya siku saba, nitanyesha mvua juu ya inchi siku makumi ine muchana na usiku, na kila kiumbe chenye uzima nilichokiumba katika dunia nitakiangamiza.”
Maana mimi niko pamoja nawe, nipate kukuokoa. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitayaangamiza kabisa mataifa yote, ambayo niliyokusambaza kati yao; lakini sitakuangamiza wewe kabisa. Nitakuazibu kadiri unavyostahili wala sitakuachilia uende bila kukuazibu. –Ni ujumbe wa Yawe.
Mimi ninawachungulia hao si kwa mema lakini kwa mabaya. Watu wote wa Yuda katika inchi ya Misri wataangamizwa kwa upanga na njaa, hakutabaki hata mutu mumoja.
Usiogope, ee Yakobo mutumishi wangu, kwa maana mimi niko pamoja nawe. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambayo nimekutawanya kati yao, lakini wewe sitakuangamiza. Nitakuazibu kadiri unavyostahili, sitakuacha bila kukuazibu.
Mupande, mupite katika mashamba yake ya mizabibu, muharibu kila kitu lakini musivimalize kabisa. Mukate matawi yake, kwa maana hayo si yangu mimi Yawe.
Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Yezereheli”, maana kisha siku chache tu, nitaiazibu jamaa ya Yehu kwa mauaji aliyofanya katika bonde la Yezereheli. Hivi nitavunja ufalme katika taifa la Israeli.
Yawe, anasema hivi: Kama vile muchungaji anavyonyanganya toka katika kinywa cha simba miguu miwili tu au kipande cha sikio la kondoo, ndivyo watu wachache tu wa Israeli wanaoishi Samaria, ambao sasa wanalalia vitanda vizuri na matandiko ya hariri watakavyobaki.
Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Muke wako atakuwa kahaba katika muji, na wana wako na wabinti zako watauawa katika vita. Inchi yako itagawanywa na kupewa wengine, nawe mwenyewe utakufia katika inchi inayohesabiwa kuwa chafu; nao Waisraeli hakika watapelekwa katika uhamisho, mbali kabisa na inchi yao.