Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 9:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Siku zinakuja ambapo wakati wa kuvuna utafuata mbio wakati wa kulima, wakati wa kukamua zabibu utafuata mbio wakati wa kupanda mizabibu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Milima itabubujika divai mupya, navyo vilima vitatiririka divai.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 9:13
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Atafunga punda wake katika muzabibu na mwana-punda wake kwenye muzabibu bora. Atafua nguo zake katika divai, na kanzu zake katika divai nyekundu.


Milima inayeyuka kama inta mbele ya Yawe, mbele ya Bwana wa dunia yote.


Furaha na shangwe zimetoweka katika shamba lenyi mavuno mengi. Kwenye mizabibu hakuna kuimba tena, wala kupiga vigelegele. Hakuna tena kukamua zabibu ndani ya vikamulio, sauti za furaha za mavuno zimekomeshwa.


Pahali pa miiba kutaota miti ya shindano, na pahali pa michongoma kutaota misunobari. Hilo litakuwa jambo litakalowakumbusha watu juu ya mambo niliyotenda mimi Yawe, kitambulisho cha milele ambacho hakitafutwa.


Watakaa humo kwa salama kabisa; watajenga nyumba na kupanda mizabibu. Wataishi bila hofu maana mataifa jirani zao ambayo yaliwauzi, mimi nitayaazibu. Hapo watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wao.


Nao watu watasema: Inchi hii iliyokuwa jangwa, sasa imekuwa kama bustani ya Edeni, nayo miji iliyokuwa ukiwa, matongo na mabomoko, sasa inakaliwa na watu, tena inazungukwa na kuta!


Nafasi ya kupepetea itajaa ngano, vikamulio vitafurika divai na mafuta.


Kupepeta ngano kutaendelea mpaka wakati wa kuvuna zabibu, na mavuno ya zabibu mpaka wakati wa kupanda mbegu. Mutakuwa na chakula tele na kuishi kwa usalama katika inchi yenu.


Bwana wetu Yawe wa majeshi, anaigusa dunia nayo inatetemeka, na wakaaji wake wanaomboleza; dunia nzima inapanda na kushuka kama vile muto Nili wa Misri unavyojaa na kupunguka.


Si ninyi munazoea kusema: ‘Kunabaki miezi mine kuwe mavuno’? Lakini mimi ninawaambia, muinue macho, muangalie mashamba; mimea imekomaa, nayo ni tayari kwa kuvunwa.


Milima ilitikisika mbele yako Yawe, mulima Sinai mbele yako Yawe, Mungu wa Israeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ