Nikasema: “Kulingana na uwezo tunaokuwa nao, tumekuwa tukiwanunua tena wandugu zetu Wayuda waliokuwa wameuzishwa kwa watu wa mataifa mengine. Lakini sasa hata munawauzisha wandugu zenu, nasi tunalazimika kuwanunua!” Basi wakanyamaza kimya, bila kuwa na la kujibu.
Huko kwako kuna watu ambao wanapokea kitulizo kwa kumwanga damu. Wanakopesha kwa kudai faida ya juu, wananyanganya mali za wenzao kwa nguvu, na kunisahau mimi kabisa! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya Waisraeli, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wameuzisha watu wa haki kuwa watumwa kwa maana hawakuweza kulipa madeni yao; na kuwauzisha wakosefu wanaoshindwa kulipa deni la muguu mumoja wa mapapa.
Mutangaze katika nyumba nzuri kule Asidodi, na katika nyumba nzuri za inchi ya Misri: Mukusanyike kwenye milima inayoizunguka inchi ya Samaria, mujionee fujo kubwa na mateso yanayofanyika kule.
Musikilize neno hili, enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria. Ninyi munaowaonea wamasikini, munaowagandamiza wakosefu, na kuwaambia waume zenu: Mutuletee divai tukunywe! Musikilize ujumbe huu: