Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 8:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Munajisemesha ndani ya mioyo yenu: Sikukuu ya mwandamo wa mwezi itakwisha wakati gani kusudi tuanze tena kuuzisha vyakula vyetu? Siku ya Sabato itakwisha wakati gani kusudi tupate kuuzisha ngano yetu? Tutapunguza vipimo, tutapandisha bei, tutadanganya watu kwa mizani zisizokuwa sawa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 8:5
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mume wake akamwuliza: “Kwa nini unataka kumwona leo? Leo si sikukuu ya mwandamo wa mwezi wala Sabato.” Akamujibu: “Si neno.”


Uwaambie Waisraeli hivi: Ninyi mutashika hakika Sabato zangu, kwa sababu hizo ni kitambulisho kati yenu na mimi kwa vizazi vyote kwamba mimi ndimi ninayewatakasa.


Mizani danganyifu ni chukizo kwa Yawe, lakini matumizi ya vipimo vya haki ni furaha kwake.


Mizani na vipimo vya kweli ni vya Yawe. Mawe yote ya kupimia katika mufuko ni kazi yake.


Mizani danganyifu ni chukizo kwa Yawe, na vipimo visivyokuwa vya haki ni kitu kibaya.


Musiniletee tena matoleo yenu yasiyokuwa na maana; ninachukizwa na sadaka yenu ya ubani. Muache kufanya sikukuu za mwandamo wa mwezi, Sabato na mikutano ya ibada; sikubali ibada zilizochanganyika na maovu.


Kama ukiacha kufanya kazi siku ya Sabato, ukiacha shuguli zako siku yangu hiyo takatifu, ukiifanya siku yangu kuwa ya furaha, ukiheshimu siku hiyo takatifu ya Yawe, ukiacha shuguli zako au kupiga domo,


Lakini ninyi mumurudilie Mungu wenu. Mushikamane na wema na haki, mumutumainie Mungu wenu siku zote.


Efuraimu ni sawa na muchuuzi anayetumia vipimo vya udanganyifu, anayependa kudanganya watu.


Munapaswa kutumia mizani ya kweli na vipimo vinavyokuwa vya kweli. Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri.


Nami nikamwuliza: Ni kitu gani hicho? Naye akanijibu: Hicho ni kikapu chenye makosa ya inchi nzima.


Yule malaika akaniambia: Mwanamuke yule ni mufano wa uovu! Kisha yule malaika akamusukumia ndani ya kikapu mwanamuke yule na kukifunika.


Munasema: Mambo haya yametuchokesha sana na munanizarau. Munaniletea sadaka za nyama muliopata kwa njia ya kunyanganya, au wanaokua vilema au wagonjwa. Basi, nipokee sadaka hizo toka katika mikono yenu?


Vilevile katika siku zenu za furaha, kama vile sikukuu za mwandamo wa mwezi na sikukuu nyingine, mutapiga baragumu hizi wakati munapotoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani. Hapo mimi Mungu wenu nitawakumbuka. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Basi, mutu asiwahukumu juu ya chakula au kinywaji, au juu ya kushika sikukuu fulani, ikiwa sikukuu ya Mwandamo wa Mwezi au siku ya Sabato.


Daudi akamwambia: “Kesho ni sikukuu ya mwandamo wa mwezi, nami nilipaswa kuwa kwenye meza kwa kula pamoja na mufalme. Lakini uniache, niende kujificha kule katika shamba mpaka siku ya tatu magaribi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ