Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 8:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Naye Yawe akaniuliza: Amosi, unaona nini? Nami nikamujibu: Ninaona kikapu cha matunda yenye kuivya. Kisha Yawe akaniambia: Mwisho umewafikia watu wangu wa Israeli. Sitavumilia tena maovu yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 8:2
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akamwambia Noa: “Nimeamua kuwaangamiza wanadamu wote kwa sababu wamejaza dunia mateso makali. Hakika, nitawaangamiza kabisa pamoja na dunia!


utukufu wake unatoweka kama ua linalonyauka; utukufu uliotawala katika bonde kwenye udongo muzuri utakuwa kama tini za mwanzo mbele ya wakati wa mavuno; mutu akiziona anazichuma na kuzikula mara moja.


Mimi nitakaa Misipa nipate kuwa musimamizi wenu mbele ya Wakaldea watakaofika kwetu; lakini ninyi muvune matunda na mukamue divai na mafuta, mujiwekee akiba ya vitu hivyo, mukae katika miji mutakayoirizi.


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


Watu walifuatilia hatua zetu, tukashindwa kupita katika barabara zetu. Mwisho wetu ulikaribia, siku zetu zilitimia, mwisho wetu ulifika.


Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema kwamba nitakomesha mezali hiyo nao hawataitumia tena katika inchi ya Waisraeli. Uwaambie kwamba wakati umefika ambapo maono yote yatatimia.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaleta upanga juu yako na kuwaua watu na nyama wako wote.


Tena akaniambia hivi: Wewe mwanadamu, maneno yote nitakayokuambia uyaweke ndani ya moyo wako, na uyasikilize vizuri.


Lakini Waisraeli watakataa kukusikiliza, maana hawataki kunisikiliza mimi. Watu wote wa Israeli ni wenye kichwa nguvu na moyo mugumu.


Mwisho umekuja! Kweli, mwisho umefika! Umewafikia ninyi!


Kisha Mungu akaniambia: Wewe mwanadamu, umeona mambo wazee wa Waisraeli wanayotenda kwa uficho, kila mutu katika chumba chake cha sanamu. Wanasema: Yawe hatuoni. Yawe ameiacha inchi.


Mungu akaniambia: Wewe mwanadamu, umeyaona mambo hayo? Hata hivyo, watu wa Yuda wanaona machukizo hayo kuwa ni kidogo. Wanajaza mateso makali katika inchi na kuzidi kunikasirikisha. Angalia jinsi wananichukiza!


Basi, Mungu akaniambia hivi: Wewe mwanadamu, unaona mambo wanayofanya, machukizo makubwa Waisraeli wanayofanya kusudi wapate kunifukuza kutoka katika hekalu langu? Tena utaona machukizo mengine makubwa zaidi.


Siku za azabu zimetimia, siku za kulipiza kisasi zimefika; Waisraeli lazima wautambue wakati huo! Ninyi munasema: Nabii ni mupumbafu; anayeongozwa na roho ni mwenda-wazimu. Munasema hivyo kwa sababu ya uovu wenu mukubwa, kwa sababu ya chuki yenu kali juu yake.


Naye akaniuliza: Amosi, unaona nini? Nikamujibu: Ninaona timazi. Kisha Yawe akasema: Ninaweka timazi kati ya watu wangu Waisraeli. Sitavumilia tena maovu yao.


Bwana wetu Yawe alinionyesha maono mengine: Niliona kikapu kilichojaa matunda yenye kuivya.


Ole wangu! Mimi ninakuwa kama muvunaji kisha wakati wa mavuno; hakuna tini za kwanzakwanza ninazotamani. Ni kama wakati wa kuchuma zabibu: hakuna hata fungu moja la zabibu la kula!


Yule malaika akaniuliza: Unaona nini? Nami nikamujibu: Ninaona kitabu kinaruka katika anga; urefu wake ni metre kenda na upana wake ni metre ine na nusu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ