Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 8:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa kilio, na nyimbo zenu za furaha kuwa maombolezo. Nitawavalisha ninyi wote magunia kwa huzuni na kunyoa vichwa vyenu upaa, kama kuomboleza kifo cha mutoto wa pekee. Na siku ya mwisho itakuwa ya uchungu mukubwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 8:10
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye akakwenda kando, akaikaa umbali wa kama metre mia moja hivi, akisema ndani ya moyo wake: “Heri nisimwone mwana wangu akikufa.” Na alipokuwa amekaa pale, mutoto akalia kwa sauti kubwa.


Akiwa anajishugulisha kwa kushibisha tumbo, Mungu atamuletea kasirani yake imutiririkie kama chakula chake.


Itawaliwe na giza kubwa sana, mawingu mazito yaifunike. Giza la muchana liitishe!


Kinubi changu kimekuwa cha kufanya kilio filimbi yangu kwa ajili ya kuomboleza.


Kwa pahali pa harufu ya marasi watatoa uvundo; kwa pahali pa mikaba mizuri watatumia kamba; kwa pahali pa nywele nzuri watakuwa na upaa; kwa pahali pa nguo nzuri watavaa magunia; uzuri wao wote utageuka kuwa haya.


Uovu wako utakuazibu; na uasi wako utakuhukumu. Ujue na kutambua kwamba ni vibaya sana kuacha Bwana wako Yawe, Mungu wako, na kutokuwa na woga wangu ndani yako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.–


Kila mutu amenyoa kichwa na ndevu zake. Wote wamejikatakata kwenye mikono na kwenye viuno wamevaa gunia.


Yawe anasema: Muvae magunia, enyi watu wangu na kugaagaa katika majivu. Muomboleze kwa uchungu, kama mutu anayemulilia mwana wake wa pekee, maana mwangamizaji atakuja, na kuwashambulia kwa rafla.


Furaha ya mioyo yetu imetoweka, michezo yetu imegeuzwa kuwa maombolezo.


Watavaa gunia, hofu itawashika, nao watapata haya na vichwa vyao vyote vitanyolewa.


Wewe mwanadamu, uwaambie wakaaji wa inchi ya Israeli kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Ni Mwisho! Mwisho umeifikia inchi yote, kutoka pande zote ine!


Kwa hiyo wakati wa mavuno nitaitwaa ngano yangu, nitaiondoa divai yangu kwa wakati wake. Nitamunyanganya nguo zangu za sufu na kitani, ambazo zilitumika kuufunika uchi wake.


Nitakomesha furaha zake zote, sikukuu zake za mwandamo wa mwezi na za Sabato, na sikukuu zote zilizoamriwa.


Mulie kama vile binti aliyevaa gunia akiombolezea kifo cha muchumba wake.


Kama mwanaume amepata upaa, yeye ni safi maana ana upaa tu.


Yawe anasema hivi: Ninachukia na kuzarau sikukuu zenu; siifurahii mikutano yenu ya kidini.


Muondoe mbele yangu kelele za nyimbo zenu! Sitaki kusikiliza muziki wa vinubi vyenu!


Siku hiyo, nyimbo za nyumba ya kifalme zitakuwa maombolezo. –Ni ujumbe wa Yawe.– Kutakuwa maiti nyingi, nazo zitatupwa fasi zote kimyakimya.


Watateketezwa kama kichaka cha miiba, wao wanaoikalia kulewa. Watateketezwa kama vile majani yenye kukauka.


Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.


Mutafanya karamu hiyo, ninyi na watoto wenu wanaume na wanawake, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ