Yawe alisimama juu ya ngazi hiyo, akamwambia: “Mimi ni Yawe, Mungu wa Abrahamu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nitakupa inchi unayoilalia wewe na wazao wako.
Kisha aliwashinda Wamoabu. Aliwapanga katika mistari mateka hao, na kuwalalisha chini. Aliamuru wale waliokuwa katika mistari miwili wauawe na wale wa mustari wa tatu waachwe wazima. Hivyo, Wamoabu wakakuwa watumishi wa Daudi na wakakuwa wanamulipa kodi.
Nitauazibu Yerusalema kama vile nilivyofanya Samaria, na mufalme Ahabu na wazao wake. Nitasafisha Yerusalema kama vile wanavyosafisha sahani na kuigeuza kisha kusafishwa.
Nitatumia sheria kama kipimo changu, nitatumia haki kama timazi. Mvua ya mawe itaufagilia mbali uongo munaoutegemea, na mafuriko yataharibu kikingio chenu.
Yawe alikusudia kuubomoa ukuta wa Sayuni; aliupima na kuhakikisha kila kitu kwamba kimeharibika; minara na kuta za inje ya muji akazifanya ukiwa, zote kwa pamoja zikaangamia.
Basi, alinipeleka huko, nami nikamwona mutu aliyeonekana anaangaa kama shaba. Katika mikono yake mutu huyo alikuwa na kamba ya kitani ya kupima nayo pamoja na ufito wa kupima nao, naye alikuwa amesimama karibu na mulango.
Maendeleo ya ujenzi wa hekalu yanaonekana madogo, na watu wanayazarau; lakini watamwona Zerubabeli akiendelea kulijenga hekalu, nao watafurahi. Sasa, juu ya hizo taa saba, yule malaika akaniambia: Ni macho saba ya Yawe yanayoona kila nafasi katika dunia.