Hivyo akasema: “Nitamuharibu kabisa katika dunia mwanadamu niliyemwumba, pamoja na nyama wa pori, viumbe vinavyotambaa na ndege wa anga. Ninasikitika kwamba niliwaumba katika dunia.”
Halafu Mungu akatuma malaika aende kuharibu Yerusalema. Lakini mbele hajafanya vile, Yawe akageuza nia yake na kumwambia malaika yule aliyetimiza maangamizi: “Basi, inatosha!” Malaika alikuwa amesimama karibu na uwanja wa kupepetea ngano wa Ornani wa kabila ya Yebusi.
Hezekia, mufalme wa Yuda, na watu wote wa Yuda hawakumwua Mika. Hezekia alimwogopa Yawe na kuomba rehema kwake. Naye Yawe akabadilisha nia yake ya kuleta hasara aliyokusudia juu yao. Lakini sisi tuko mbio kwa kujiletea hasara wenyewe.
Kama ninyi mutabaki katika inchi hii, basi, nitawasimamisha, wala sitawaharibu; nitawaotesha wala sitawaongoa; kwa maana nitabadilisha nia kwa sababu ya hasara niliyowatendea.
Ewe Efuraimu, ninaweza kukuacha namna gani? Ninaweza kukutupilia, ewe Israeli namna gani? Nitaweza namna gani kukufanya kama muji wa Adama? Nitaweza namna gani kukutendea kama Zeboimu! Ninazuizwa na moyo wangu; huruma yangu imezidi kuwa motomoto.
Munapasua nguo zenu kwa kuonyesha huzuni, lakini inafaa mioyo yenu ipasuke vilevile. Murudilie Yawe, Mungu wenu. Yeye amejaa huruma na rehema, hakasiriki upesi, ni mwingi wa wema, na tayari kubadilisha nia zake kusudi asiazibu.