Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 7:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Muke wako atakuwa kahaba katika muji, na wana wako na wabinti zako watauawa katika vita. Inchi yako itagawanywa na kupewa wengine, nawe mwenyewe utakufia katika inchi inayohesabiwa kuwa chafu; nao Waisraeli hakika watapelekwa katika uhamisho, mbali kabisa na inchi yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 7:17
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mufalme wa Asuria aliuteka muji wa Samaria na kuwapeleka watu wa Israeli katika uhamisho mpaka Asuria. Wamoja kati yao akawaweka katika muji wa Hala, wengine karibu na muto Habori, muto Gozani na wengine katika miji ya Wamedi.


Alifukuza mataifa mbele yao, akatoa inchi zao zikuwe mali ya Israeli, akaikalisha makabila ya Israeli katika mahema zao.


Watoto wao wachanga watapondwapondwa mbele yao, watanyanganywa nyumba zao, na watalala na wake zao kwa kinguvu.


na kukuzungushazungusha, kisha atakutupa kama mupira mpaka katika inchi pana. Huko utakufia karibu na magari yako ya vita unayojivunia, wewe unayezaraulisha nyumba ya bwana wako.


Na hao ambao waliowatabiria mambo hayo, maiti zao zitatupwa katika barabara za Yerusalema wakiuawa kwa njaa na vita, wala hakutakuwa mutu wa kuwazika wao wenyewe, wake zao, wabinti zao na wana wao. Mimi nitawabebesha lazima ya uovu wao wenyewe.


Na kwa upande wako, wewe Pashuri, pamoja na watu wote wanaokaa ndani ya nyumba yako, mutapelekwa katika utumwa. Hakika mutakwenda Babeli na huko ndiko utakapokufia na kuzikwa, pamoja na warafiki zako wote uliowatabiria uongo.


Nyuma ya pale nabii Hanania alipovunja nira kutoka katika shingo la nabii Yeremia, neno la Yawe lilimufikia Yeremia kusema hivi:


Kwa hiyo Yawe anasema hivi: Nitakuondoa katika dunia. Mwaka huuhuu utakufa, kwa sababu umewasukuma watu wamwasi Yawe.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi juu ya Ahabu, mwana wa Kolaya na juu ya Zedekia mwana wa Masea, ambao wanawatabiria uongo kwa jina lake: Nitawatoa katika mikono ya Nebukadneza, mufalme wa Babeli, naye atawaua waziwazi mbele ya macho yenu.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Umejiruhusu kutuma barua kwa wakaaji wote wa Yerusalema na kwa kuhani Zefania, mwana wa Masea na kwa makuhani wengine wote. Katika barua hiyo, ulimwambia Zefania hivi:


Wanawake wetu wanatendewa kwa kinguvu katika Sayuni, na wabinti wetu katika miji ya Yuda.


Yawe aliniambia: Vile ndivyo Waisraeli watakavyokula mukate wao muchafu wakiwa kati ya mataifa ninakowapeleka.


Hawatakaa katika inchi ya Yawe. Watu wa Efuraimu watarudi katika utumwa kule Misri. Watakula vyakula vichafu kule Asuria.


Kwa hiyo mutakuwa wa kwanza kwenda katika uhamisho, na karamu za wenye kustarehe zitatoweka.


Anachosema ni hiki: Yeroboamu atakufa kwa upanga nao Waisraeli watapelekwa katika uhamisho, mbali kabisa na inchi yao.


Bwana wetu Yawe alinionyesha maono mengine: Niliona kikapu kilichojaa matunda yenye kuivya.


Nilimwona Yawe akisimama pembeni ya mazabahu, naye akaniamuru: Piga zile nguzo za hekalu mpaka misingi yake itikisike. Uvunje zile nguzo ziwaangukie watu juu ya vichwa. Wale watakaobaki nitawaua kwa upanga; hakuna hata mumoja wao atakayeponyoka, hakuna atakayetoroka.


Ninauangalia ufalme wenye zambi, na nitauangamiza kabisa kutoka katika dunia. Lakini sitawaangamiza wazao wote wa Yakobo. –Ni ujumbe wa Yawe.


Enyi watu wa Yuda, munyoe vichwa vyenu kwa kuwaomboleza watoto wenu wapenzi; mupanue upaa wenu ukuwe mupana kama wa tai, maana watoto wenu watawaacha kwenda katika uhamisho.


Yawe atayakusanya mataifa yote kwa kuushambulia Yerusalema. Muji utakamatwa, nyumba zenu zitatekwa, na wanawake wenu watakamatwa kwa kinguvu. Nusu ya wakaaji wa muji watapelekwa katika uhamisho, lakini nusu itakayobaki haitaondoshwa inje ya muji.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ