Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 7:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Basi, Amazia kuhani wa muji wa Beteli, akamupelekea mufalme Yeroboamu wa Israeli habari hii: Amosi analeta fitina juu yako katika ufalme wa Israeli. Hotuba zake ni hatari kwa inchi hii.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 7:10
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wandugu zake wakamwuliza: “Unataka kutuambia kwamba utatutawala? Au utakuwa na mamlaka juu yetu?” Basi, wakazidi kumuchukia kwa sababu ya ndoto na maneno yake.


Yeroboamu hakuuacha upotovu wake; aliendelea kuchagua watu wa kawaida kuwa makuhani, watumike kwa nafasi ya kutambikia juu ya vilima. Mutu yeyote aliyejitolea, alimutakasa kuwa kuhani wa nafasi ya kutambikia kule juu ya vilima.


Ahabu alipomwona Elia, alisema: “Hakika ni wewe unayetaabisha Waisraeli?”


Kisha, watu wakasema: Tuende tufanye shauri baya juu ya Yeremia, maana hatukosi makuhani wa kutufundisha. Vilevile hatukosi watu wenye hekima wa kutushauria na manabii wa kututangazia ujumbe wa Mungu! Mukuje tumushitaki kufuatana na maneno yake mwenyewe, wala tusiyatilie maana mambo yote anayosema.


Waliposikia maneno hayo yote, waliangaliana kwa hofu. Wakamwambia Baruku: Tunapaswa kumwelezea mufalme maneno haya yote.


Wakubwa wakamwambia mufalme: Inafaa mutu huyu auawe kwa maana anawavunja moyo waaskari ambao wameachwa katika muji huu na watu wote kwa jumla, kwa kusema maneno kama hayo. Yeye hawatakii watu hawa mema lakini mabaya.


Haya ni maneno ya Amosi, mumoja wa wachungaji wa nyama wa muji wa Tekoa. Mungu alimufunulia Amosi mambo haya yote juu ya inchi ya Israeli miaka miwili mbele ya tetemeko la inchi, wakati Uzia alipokuwa mufalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi alipokuwa mufalme wa Israeli.


Siku nitakapowaazibu Waisraeli kwa sababu ya makosa yao, nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli. Nitazikata pembe za kila mazabahu na kuziangusha chini.


Ninyi munawachukia wanaotetea haki na wenye kusema ukweli katika tribinali.


Lakini musinitafutie kule Beteli wala musiende Gilgali wala musivuke kwenda Beri-Seba. Maana wakaaji wa Gilgali, hakika watapelekwa katika uhamisho, na Beteli utaangamizwa!


Anachosema ni hiki: Yeroboamu atakufa kwa upanga nao Waisraeli watapelekwa katika uhamisho, mbali kabisa na inchi yao.


Yesu akaingia ndani ya hekalu. Alipokuwa akifundisha, wakubwa wa makuhani pamoja na wasimamizi wa watu wakamufikia na kumwuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka yale?”


Wakaanza kumushitaki, wakisema: “Tulimukuta mutu huyu akiwashawishi watu wa taifa letu kufanya uasi. Yeye alikuwa akiwaambia kwamba wasilipe kodi kwa Mufalme wa Roma. Na zaidi ya hii anasema kwamba yeye ndiye Kristo, Mufalme aliyengojewa.”


Tumetambua kwamba mutu huyu ni wa hatari sana, ameanzisha fujo kati ya Wayuda wote katika dunia. Tena yeye ni mukubwa wa chama cha Wanazareti.


akiwaambia: “Tuliwakataza kwa nguvu musifundishe tena kwa jina la mutu huyu. Na sasa mumeeneza mafundisho yenu katika Yerusalema yote, nanyi munataka kutubebesha lazima ya kifo chake.”


Wajumbe wa Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kumusagia Stefano meno.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ