Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 6:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Bwana wetu Yawe ameapa kwa nafsi yake: Ninachukizwa sana na kiburi cha wazao wa Yakobo; tena ninachukia nyumba zao nzuri sana. –Ni ujumbe wa Yawe.– Muji wao na vyote vinavyokuwa ndani yake nitavipatia waadui zake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 6:8
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

akamwambia: “Yawe anasema hivi: Nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe kwamba kwa sababu umefanya hivi, wala haukuninyima mwana wako wa pekee,


Hasira ya Yawe ikawawakia watu wake, akachukizwa sana na hao waliokuwa mali yake.


Ametuwezesha kuwashinda watu wa mataifa, ameyaweka mataifa chini ya mamlaka yetu.


Kama ningesikia njaa, singekuambia wewe, maana ulimwengu na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vyangu.


Mungu alipoona hayo, akawaka hasira; akamukataa Israeli kabisa.


Kumwogopa Yawe ni kuchukia uovu. Ninachukia kiburi, majivuno maisha mabaya, na luga mbaya.


Ole wa Samaria, muji unaokuwa kama taji juu ya bonde kwenye udongo muzuri. Walevi wa ajabu wa Efuraimu wanajivuna kwa ajili yake, lakini utukufu wake utatoweka kama ua linalonyauka!


Wachaguliwa wangu wamenigeuka, wamekuwa kama simba katika pori, wameningurumia mimi; ndiyo maana ninawachukia.


Wewe unayesema: Nitajijengea nyumba kubwa, yenye vyumba vikubwa vya magorofi. Kisha unaifanyia madirisha, ukafunika kuta zake kwa mbao za mierezi, na kuipaka rangi nyekundu!


Lakini kama hamutatii maneno haya, ninaapa kwa nafsi yangu mwenyewe kwamba nafasi hii itakuwa mabomoko. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini musikilize neno la Yawe, enyi watu wote wa Yuda munaokaa katika inchi ya Misri. Yawe anasema hivi: Ninaapa kwa jina langu kubwa kwamba hakuna mutu yeyote wa Yuda katika inchi yote ya Misri atakayelitumia jina langu kwa kuapa nalo akisema: Kama vile Bwana wangu Yawe anavyoishi.


Maana nimeapa kwa nafsi yangu kwamba muji wa Bosira utakuwa kitisho na mushangao, utakuwa uharibifu na kutumiwa kama mufano wa laana; vijiji vyote vitakuwa mabomoko siku zote. –Ni ujumbe wa Yawe.


Yawe wa majeshi ameapa kwa nafsi yake: Hakika nitakujaza na watu kama vile nzige, nao watapiga vigelegele vya ushindi juu yako.


Yawe amekuwa kama adui, ameangamiza watu wa Israeli; ameharibu nyumba zake kubwa zote, amevibomoa vikingio vyake. Amewazidishia watu wa Yuda kilio na maombolezo.


Uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitalichafua hekalu langu, hiyo nyumba ambayo munajivunia na kuitegemea na ambao munafurahi sana kuiona.


Upanga utavuma katika miji yao, utavunjavunja miimo ya milango yake na kuwaangamiza katika kuta zao.


Nitaweka makao yangu kati yenu, wala sitawaachilia.


Nitaharibu pahali penu pa ibada kule juu ya milima, nitabomoa mazabahu zenu za kufukizia ubani, na kutupa maiti zenu juu ya sanamu za miungu yenu. Roho yangu itawachukia kabisa.


Hawajui kabisa kutenda mambo yanayokuwa sawa! –Ni ujumbe wa Yawe.– Wamejaza nyumba zao nzuri na vitu vya wizi na mateso.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Waadui wataizunguka inchi yenu, wataharibu kuta zako, na kuziteka nyumba zao nzuri.


Bwana wetu Yawe Mutakatifu ameapa: Siku zinakuja ambapo watu watawakokota kwa ndoana kubwa, kila mumoja wenu kama samaki kwenye ndoana.


Yawe anasema hivi: Ninachukia na kuzarau sikukuu zenu; siifurahii mikutano yenu ya kidini.


Siku hiyo, nyimbo za nyumba ya kifalme zitakuwa maombolezo. –Ni ujumbe wa Yawe.– Kutakuwa maiti nyingi, nazo zitatupwa fasi zote kimyakimya.


Yawe, utukufu wa Yakobo, ameapa: Hakika, sitayasahau matendo yao maovu.


Kwa muda wa mwezi mumoja, nikaua wachungaji watatu wabaya. Tena uvumilivu wangu kwa kondoo ukaniishia, nao kwa upande wao, wakanichukia.


Yawe aliona jambo hilo akawaacha; aliwakataa watoto wake, wanaume na wanawake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ