Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 6:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ninyi munajaribu kuifukuza ile siku mbaya. Lakini munaukaribisha utawala wa mateso.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 6:3
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe hauwezi kushirikiana na waamuzi wapotovu, wanaotunga masharti za kutetea maovu.


Kwa vile uovu hauazibiwi haraka, mioyo ya wanadamu inakusudia kutenda mabaya.


Ulijisemesha ndani ya moyo: “Nitakuwa malkia milele”, nawe haukufikiri juu ya mambo yanayotokea, wala kuwaza juu ya mwisho wake.


Wao wanaambiana hivi: Mukuje, tuende kutafuta divai; mukuje tukunywe tushibe kinywaji kikali! Kesho itakuwa kama leo, tena itakuwa sikukuu kubwa zaidi.


Wale waliokula vyakula vinono wanakufa na njaa katika barabara. Waliolelewa na kuvalishwa namna ya kifalme wanafukua kwa mikono kwenye yalala.


Wewe mwanadamu: Kwa nini mezali hii inatajwa katika inchi ya Waisraeli: Siku zinakuja na kupita, lakini maono ya nabii hayatimii?


Wewe mwanadamu, Waisraeli wanafikiri kwamba maono yako yanahusu siku za nyuma sana, na unabii wako unahusu nyakati za mbali sana!


Basi, kukasikilika sauti za kundi la watu wasiojali kitu, kundi la wanaume walevi walioletwa kutoka katika jangwa. Waliwavalisha hao wanawake vikomo kwa mikono yao na taji nzuri juu ya vichwa vyao.


Hawajui kabisa kutenda mambo yanayokuwa sawa! –Ni ujumbe wa Yawe.– Wamejaza nyumba zao nzuri na vitu vya wizi na mateso.


Mutangaze katika nyumba nzuri kule Asidodi, na katika nyumba nzuri za inchi ya Misri: Mukusanyike kwenye milima inayoizunguka inchi ya Samaria, mujionee fujo kubwa na mateso yanayofanyika kule.


Maana mimi ninajua wingi wa makosa yenu na ukubwa wa zambi zenu; ninyi munawatesa watu wema, munapokea kituliro na kuzuia wakosefu wasipate haki katika tribinali.


Ole kwenu ninyi munaoingojea kwa hamu siku ya Yawe! Kwa nini munaitaka sana siku hiyo? Siku hiyo, itakuwa siku ya giza na si ya mwangaza!


Farasi wanaweza kukimbia katika mawe makubwa? Watu wanaweza kulima bahari na ngombe? Lakini ninyi mumeigeuza sheria kuwa sumu, na tunda la haki kuwa uchungu.


Wenye zambi kati ya watu wangu, watakufa katika vita. Hao ndio wanaosema: Hasara haitatufikia wala kutupata!


Watajiri wa miji ni watesaji wakali kabisa, wakaaji wake wanasema uongo, kila neno wanalosema ni udanganyifu.


Lakini kama mutumishi yule ni mutu mubaya, atajisemesha yeye mwenyewe kwamba bwana wake anakawia,


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


na kusema: “Aliahidi kwamba atakuja! Sasa yeye yuko wapi? Kwa maana, tangia kufa kwa babu zetu mambo yote yanaendelea kubakia sawa vile yalivyokuwa tangu kuumbwa kwa dunia.”


Kwa muda wa saa moja tu utajiri mwingi kama huu umeharibishwa.” Waongozi wote wa mashua na wasafiri wao, nao wote wanaofanya kazi ndani ya mashua na wote wanaochuuza kwa njia ya bahari walisimama kwa mbali.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ