Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 6:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Ninyi munashangilia juu ya muji wa Bure na kusema mumeuteka muji wa Nguvu kwa nguvu zenu wenyewe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 6:13
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Yoasi akamushinda Beni-Hadadi mara tatu na kuikomboa miji yote iliyotekwa wakati wa utawala wa Yoahazi, baba ya Yoasi.


Aliikomboa inchi yote iliyokuwa mali ya Israeli, kutokea Pito la Hamati mpaka bahari ya Chumvi. Hivi ndivyo Yawe alivyoahidi kwa njia ya mutumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gati-Heferi.


sikupata kufurahia wingi wa utajiri wangu au kujivunia mapato mengi ya mikono yangu.


Nimefurahia kuangamia kwa adui yangu, au kufurahi alipopatwa na hasara?


Tegemeo lao linavunjika, tumaini lao ni utando wa buibui.


Wanaegemea nyumba yao lakini haitasimama, wanaishikilia lakini haidumu.


Wafalme wa dunia wanajitayarisha, watawala wanashauriana pamoja kumwasi Yawe na muchaguliwa wake.


Inchi ikitetemeka na vyote vinavyokuwa ndani yake, mimi ndiye ninayeimarisha misingi yake.


Ninawaambia wenye kiburi: ‘Mwache kiburi’, na waovu: ‘Musiote mapembe!


Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.


Katika siku za utawala wa Ahazi mwana wa Yotamu na mujukuu wa Uzia, wa inchi ya Yuda, Resini, mufalme wa Aramu, na Peka mwana wa Remalia, mufalme wa Israeli, walienda kuushambulia Yerusalema, lakini hawakuweza kuunyanganya.


Umwambie akuwe macho, atulie na asiogope wala asivunjike moyo, kwa sababu ya hasira kali ya mufalme Resini wa Aramu, na ya mwana wa Remalia. Hao wawili ni kama tu moshi wa kuni zinazozimika.


Kwa sababu watu hawa wameyakataa maji ya Siloa yanayotiririka polepole, wakatetemeka mbele ya mufalme Resini na mufalme Peka mwana wa Remalia,


Enyi wanyanganyi wa mali yangu, ijapokuwa munafurahi na kushangilia, munarukaruka kama mwana-ngombe anayepepeta ngano, na kulia kama farasi dume,


Anayetaka kujivuna, ajivune kwamba ananifahamu mimi, kwamba anajua kwamba mimi Yawe ninatenda mema, ninafanya mambo ya haki kufuatana na sheria yangu katika dunia. Watu wa namna hiyo ndio wanaonipendeza. –Ni ujumbe wa Yawe.


Umwambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana na wewe mufalme wa Misri, wewe mamba unayelala ndani ya muto Nili! Wewe unafikiri kwamba muto Nili ni wako, kwamba wewe ndiwe uliyeufanya!


Kwa sababu umesema kwamba muto Nili ni wako, kwamba ndiwe uliyeufanya, basi, inchi yako, Misri, itakuwa tupu na jangwa. Halafu watu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!


Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


Mungu, Yawe akaamuru mumea uote na kukomaa. Akauotesha kwa kumupatia Yona kivuli cha kumupunguzia taabu aliyokuwa nayo. Yona akaufurahia sana mumea huo.


Siku hiyo, hautapata haya kutokana na matendo yako ya kuniasi, maana nitawaondoa kati yako wale wanaojivuna na kujitukuza, nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.


Kweli, kweli ninawaambia: mutalia na kusikitika, lakini watu wa dunia watafurahi. Mutahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.


Lakini sasa munajivuna na kujisifu. Majivuno yote ya namna hii ni mabaya.


Wakaaji wa dunia watafurahi kwa ajili ya kifo chao na kushangilia. Watatumiana zawadi, kwa maana manabii hawa wawili waliwasumbua sana wakaaji wa dunia.


Wakatoka na kwenda kwenye mashamba yao ya mizabibu, wakachuma zabibu halafu wakazikamua, wakatengeneza divai wakafanya sikukuu. Wakaingia kwenye nyumba ya mungu wao wakakula na kunywa, kisha wakamutukana Abimeleki.


Sanduku la Agano la Yawe lilipofika katika kambi Waisraeli wote walishangilia kwa furaha, hata inchi yote ikatikisika.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ