Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 6:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Na mujomba wa yule aliyekufa atakapokuja kuitoa maiti inje aichome, akimwuliza yeyote atakayekuwa ndani pembeni ya nyumba: Kuna mutu mwingine pamoja nawe? Atajibiwa: Hakuna! Naye atamwambia: Nyamaza kimya! Tusilitaje hata jina la Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 6:10
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Yosia alipogeuka akaona makaburi juu ya kilima. Aliagiza mifupa ifukuliwe kutoka makaburi na kuichoma juu ya mazabahu. Basi akachafua mazabahu sawasawa na neno la Yawe ambalo mutu wa Mungu alilitangaza, nabii ambaye alitabiri matukio haya.


Mbele hata hajamaliza kusema, mufalme akafika, akasema: “Mabaya haya yametoka kwa Yawe! Nitangojea nini tena kutoka kwake?”


Wote, wakubwa kama vile wadogo, watakufa katika inchi hii; nao hawatazikwa, wala hakuna atakayeomboleza juu yao. Hakuna atakayejikatakata wala kunyolewa upaa kwa ajili ya kifo chao.


Lakini musikilize neno la Yawe, enyi watu wote wa Yuda munaokaa katika inchi ya Misri. Yawe anasema hivi: Ninaapa kwa jina langu kubwa kwamba hakuna mutu yeyote wa Yuda katika inchi yote ya Misri atakayelitumia jina langu kwa kuapa nalo akisema: Kama vile Bwana wangu Yawe anavyoishi.


Sema: Huu ni ujumbe wa Yawe: Maiti za watu zinalala chini kila pahali kama malundo ya mboleo katika mashamba, kama miganda iliyoachwa na muvunaji, wala hakuna anayeikusanya.


Na sasa, enyi Waisraeli, Bwana wenu Yawe anawaambia hivi: Muendelee kuziabudu sanamu zenu za miungu, kama hamunisikilizi; lakini mutalazimishwa kuacha kulikufuru jina langu takatifu kwa sadaka na sanamu zenu.


Uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitalichafua hekalu langu, hiyo nyumba ambayo munajivunia na kuitegemea na ambao munafurahi sana kuiona.


Basi, kutakuwa wakati mubaya ambao hata mwenye hekima atanyamaza.


Siku hiyo, nyimbo za nyumba ya kifalme zitakuwa maombolezo. –Ni ujumbe wa Yawe.– Kutakuwa maiti nyingi, nazo zitatupwa fasi zote kimyakimya.


Basi, Haruni akafanya kama vile alivyoambiwa na Musa. Akatwaa chetezo chake na kukimbia mpaka katikati ya watu waliokuwa wamekusanyika pamoja. Alipoona kwamba pigo limekwisha kuanza, akatia ubani katika chetezo na kuwafanyia watu upatanisho.


mashujaa wote waliondoka, wakasafiri usiku kucha, wakaondoa mwili wa Saulo na miili ya wana wake kutoka ukuta wa Betisani, wakakuja nayo mpaka Yabesi na kuiteketeza kwa moto kule.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ