Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 6:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ole kwenu ninyi munaostarehe kule Sayuni, nanyi munaoishi katika usalama kwenye mulima Samaria! Ninyi munaonekana kuwa waongozi wa taifa kubwa, ambao Waisraeli wote wanawategemea.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 6:1
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alinunua mulima wa Samaria kwa vikoroti elfu sita vya feza kutoka kwa mutu mumoja anayeitwa Semeri, akajenga muji wenye kuta juu yake. Muji wenyewe akauita Samaria, kwa heshima ya Semeri aliyekuwa mwenyeji wa mulima huo hapo zamani.


Tumeshiba muda murefu mazarau ya watajiri, nayo masimango ya wenye kiburi.


Maana wajinga wanajiua kwa kiburi chao, wapumbafu wanajiangamiza kwa kufanikiwa kwao.


Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa, wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema: Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali? Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?


Israeli, ulikuwa wangu wa pekee, kama malimbuko ya shamba langu. Wote waliokukula walibeba hukumu, wakipatwa na hasara. –Ni ujumbe wa Yawe.


Moabu amestarehe tangu ujana wake, ametulia kama divai katika mutungi. Hajamimiliwa toka chombo kimoja katika chombo kingine, hajapata kupelekwa katika uhamisho. Kwa hiyo angali na onjo yake, harufu yake nzuri haijabadilika hata kidogo.


Simama uende kulishambulia taifa linalostarehe, taifa linaloishi kwa usalama. –Ni ujumbe wa Yawe.– Taifa hilo halina milango wala vifungio vya chuma; ni taifa ambalo liko peke yake.


Nitawaendea wakubwa niongee nao; bila shaka, wao wanajua mapenzi ya Yawe; wanajua sheria ya Mungu wao. Lakini wote ni sawa. Wamevunja nira yao, wamekata minyororo yao.


Musitumainie maneno haya ya udanganyifu mukisema: Hili ni hekalu la Yawe, hekalu la Yawe, hakika hili ni hekalu la Yawe.


Namna gani muji uliokuwa umejaa watu, sasa unakaa peke yake! Ulikuwa na utukufu kati ya mataifa, sasa umekuwa kama mama mujane. Ulikuwa kama binti wa mufalme kati ya miji, sasa umekuwa mutumwa.


Kati ya mataifa yote katika ulimwengu, ni ninyi tu niliowachagua. Kwa hiyo nitawaazibu ninyi, kwa sababu ya uovu wenu wote.


Mutangaze katika nyumba nzuri kule Asidodi, na katika nyumba nzuri za inchi ya Misri: Mukusanyike kwenye milima inayoizunguka inchi ya Samaria, mujionee fujo kubwa na mateso yanayofanyika kule.


Musikilize neno hili, enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria. Ninyi munaowaonea wamasikini, munaowagandamiza wakosefu, na kuwaambia waume zenu: Mutuletee divai tukunywe! Musikilize ujumbe huu:


Kwa hiyo nitawapeleka katika uhamisho, mbali kuliko Damasiki! –Ni Yawe anayesema, ambaye jina lake ni Mungu wa majeshi.


Wale wanaoapa kwa mungu wa uongo wa Samaria na kusema “Kwa nafsi ya mungu wako ee Dani” au “Kwa nafsi ya mungu wa Beri-Seba”, wote wataanguka na hawatasimama tena hata kidogo.


Wenye zambi kati ya watu wangu, watakufa katika vita. Hao ndio wanaosema: Hasara haitatufikia wala kutupata!


Sasa musikilize, enyi wakubwa wa wazao wa Yakobo, musikilize, enyi watawala wa wazao wa Israeli! Ninyi ndio munaopaswa kujua namna ya kufuata sheria ya Mungu.


Wakati huo nitauchunguza Yerusalema kwa taa, nitawaazibu wanaoishi wakitulia kama machicha ya divai, wote ambao wanasema kati yao: Yawe hatafanya kitu: chema au kibaya.


Kwa mapenzi yake mwenyewe alitupatia sisi uzima kwa njia ya ujumbe wa kweli, kusudi tupate kuwa kama mavuno ya kwanza katikati ya viumbe vyake.


Mumeishi katika utajiri na kujifurahisha katika maisha yenu katika dunia. Mumejinenepesha kwa kuwa tayari kwa siku ya kuchinjwa.


Mumutolee masumbuko yenu yote kwa maana yeye anawashugulikia.


Basi, watu hao watano wakaondoka, wakaenda Laisi. Waliwaona watu walioishi kule, na jinsi walivyokaa kwa usalama kama vile watu wa Sidona. Walikuwa watu watulivu wasiokuwa na wasiwasi na hawakupungukiwa mahitaji yoyote katika inchi. Walikuwa mbali na watu wa Sidona, na hawakukuwa na shuguli yoyote na watu wengine.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ