Mufalme alifuata maagizo ya nabii na kufungua dirisha ambalo lilielekea Aramu. Elisha akatoa amri: “Tupa mushale!” Mara tu mufalme alipotupa mushale, nabii akasema: “Wewe ndio mushale wa Yawe, ambao kwa njia yake atapata ushindi juu ya Waaramu. Utapigana na Waaramu kule Afeki mpaka uwashinde.”
Hata kama mukiwashinda waaskari wote wa Wakaldea wanaopigana nanyi na kunabaki tu katika mahema yao wale walioumizwa, hao watasimama na kuuteketeza muji huu kwa moto.
walizimisha moto mukali, waliponyoka kuuawa kwa upanga. Walikuwa wazaifu, lakini wakapata nguvu; walikuwa shujaa katika vita na kushinda majeshi ya kigeni.