Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 5:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yawe anawaambia Waisraeli hivi: Munitafute mimi nanyi mutaishi!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 5:4
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote na kutenda mazuri mbele yako.” Hezekia akalia kwa uchungu sana.


“Nawe Solomono mwana wangu, umujue Mungu wa baba yako, na umutumikie kwa moyo wako wote na kwa nia nzuri; yeye Yawe anachunguza mioyo na anafahamu mipango na mafikiri ya mwanadamu. Ukimutafuta yeye, utamwona; lakini ukimwacha, atakutupilia mbali milele.


naye akatoka kwenda kukutana na mufalme Asa, akamwambia: “Unisikilize, ee Asa na watu wote wa kabila la Yuda na la Benjamina! Yawe yuko pamoja nanyi, ikiwa mutakuwa pamoja naye. Mukimutafuta, mutamupata, lakini mukimwacha, naye atawaacha.


Yosafati akashikwa na woga, akamwomba Yawe amwongoze. Akatangaza kwamba watu wote katika inchi ya Yuda wafunge kula.


Watu wakakuja Yerusalema kutoka miji yote ya Yuda, wakakusanyika kwa kumwomba Yawe awasaidie.


Katika mwaka wa ine wa utawala wake, mufalme Yosia, akiwa bado kijana, alianza kumwabudu Mungu wa Daudi, babu yake. Kisha alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili alianza kusafisha inchi ya Yuda na Yerusalema kwa kuharibu pahali pa kutambikia miungu mingine, sanamu za Ashera, na sanamu zingine za kuchonga na za kuyeyusha.


Yawe anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni aone kama kuna yeyote mwenye akili, kama kuna yeyote anayemutafuta Mungu.


Kwa sababu yako ninakusifu katika kusanyiko kubwa la watu; nitatimiza ahadi zangu mbele ya wanaomwabudu.


Moyo wangu unaniambia: “Kuja umutafute Mungu!” Basi, ninakutafuta, ee Yawe.


Jambo hili litamupendeza Yawe zaidi, kuliko kumutolea sadaka ya ngombe, kuliko kumutolea ngombe dume muzima.


Wanyenyekevu wataona hayo na kufurahi; wanaomutafuta Mungu watapata moyo.


Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!


Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.


Yeremia akamujibu: Hautatolewa kwao. Wewe sasa utii kile Yawe anachosema, kama ninavyokuambia, na mambo yote yatakuendekea vema, na maisha yako yataokolewa.


Mupande haki kwa faida yenu, nanyi mutavuna wema; mulime mashamba yaliyoachwa, maana wakati wa kutafuta Yawe umefika kusudi awanyeshee haki kama mvua.


Mutafute Yawe, nanyi mutaishi! Kama sivyo, atawatokea wazao wa Yosefu kama moto; moto utawateketeza wakaaji wa Beteli na hakuna mutu atakayeweza kuuzimisha.


Mutafute Yawe, enyi wanyenyekevu wote katika inchi, enyi munaozitii amri zake. Mutafute haki, mutafute unyenyekevu; labda mutaiponyoka siku ya kasirani ya Yawe.


Kwa maana kila mutu anayeomba, anapewa; naye anayetafuta, anapata, naye anayepiga hodi, anafunguliwa.


akawaambia: “Muweke ndani ya mioyo yenu maneno yote ambayo ninawapa leo. Muwaamuru watoto wenu kusudi wafuate kwa uaminifu maneno yote ya sheria hii.


Maana sheria hii si maneno matupu lakini ni uzima wenu; kwa njia ya sheria hii, mutaishi maisha marefu katika inchi munayokwenda kurizi, ngambo ya muto Yordani.”


Kisha kutoka humohumo katika inchi mutamutafuta Yawe, Mungu wenu, nanyi mutamupata kama mukimutafuta kwa moyo wote na roho yote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ