Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 5:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Maana Bwana wetu Yawe anasema: Itakuwa hivi: juu yenu ninyi Waisraeli: Watu elfu moja wanatoka katika muji kwenda kupigana lakini watarudia watu mia moja tu; wataondoka watu mia moja wa kijiji kimoja lakini watu kumi tu wataponyoka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 5:3
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ngombe wetu wakuwe na afya na nguvu, kusitokwe mimba wala kukosa kuibeba. Kusikuwe tena kilio katika mitaa yetu.


Yawe wa majeshi asingetuachia watu wachache, tungekwisha kuwa kama watu wa Sodoma tungekuwa na hali ileile ya Gomora.


Maana, hata kama sasa Waisraeli ni wengi kama muchanga wa bahari, ni wachache tu watakaorudi. Maangamizi yamepangwa yafanyike, nayo yatafanyika kwa haki tu.


Hata kukibaki sehemu moja ya kumi ya watu, nao vilevile watateketezwa. Hao watakuwa kama muti wa muvinje au wa mwalo ambao shina lake limebaki kisha kukatwa. Shina hilo ni mbegu takatifu ya mwanzo mupya.


Lakini nitawaacha wachache waepuke vita, njaa na ugonjwa mukali; kusudi hao waweze kuwaelezea watu wa mataifa wanamoishi jinsi walivyotenda mabaya. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Kama wakibaki watu kumi katika nyumba moja, wote watakufa.


Isaya alisema kwa sauti juu ya Waisraeli: “Ijapokuwa Waisraeli ni wengi kama muchanga wa bahari, ni wachache tu watakaookolewa.


Ijapokuwa ninyi ni wengi kama nyota za mbinguni, lakini mutakuwa wachache tu kwa sababu hamukutii sauti ya Yawe, Mungu wenu.


Kama vile Yawe alivyopendezwa kuwafanikisha na kuwafanya kuwa wengi, ni vile vile Yawe atapendezwa kuwaletea hasara na kuwaangamiza. Nanyi mutaondolewa katika inchi hiyo ambayo munakwenda kuirizi.


Yawe atawatawanya kati ya mataifa mengine, na ni wachache tu wenu watakaobakia huko ambako Yawe atawafukuzia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ