Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 5:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Kwa hiyo nitawapeleka katika uhamisho, mbali kuliko Damasiki! –Ni Yawe anayesema, ambaye jina lake ni Mungu wa majeshi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 5:27
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hakika, tangu sasa, Yawe atawapiga watu wa Israeli, nao watatikisika kama unyasi unavyotikiswa ndani ya muto. Atawaongoa kutoka inchi hii nzuri aliyowapa babu zao, na kuwatawanya mbali, ngambo ya muto Furati, kwa sababu wamemukasirikisha Yawe kwa kujitengenezea sanamu za Ashera.


Wakati wa utawala wa Peka mufalme wa Israeli, Tigilati-Pileseri, mufalme wa Asuria, aliteka miji ya Iyoni, Abeli-Beti-Maka, Yanoa, Kadesi na Hazori, pamoja na inchi za Gileadi, Galilaya na Nafutali na kuwahamisha wakaaji wake kwenda Asuria.


mpaka kwa mwisho Yawe akawafukuza kutoka mbele yake, kama vile alivyokuwa amesema kupitia kwa watumishi wake wote manabii. Kwa hiyo watu wa Israeli walipelekwa katika uhamisho kutoka katika inchi yao wenyewe mpaka Asuria ambako wanakaa hata sasa.


Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mufalme wa Asuria aliuteka muji wa Samaria na kuwapeleka watu wa Israeli katika uhamisho mpaka Asuria. Wamoja kati yao akawaweka katika muji wa Hala, wengine karibu na muto Habori, muto Gozani na wengine katika miji ya Wamedi.


Hapo Yeremia akamwambia Zedekia: Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama ukijitoa mwenyewe na kujitia katika mikono ya wakubwa wa mufalme wa Babeli, utayaokoa maisha yako na muji hautateketezwa kwa moto; nawe pamoja na jamaa yako mutaendelea kuishi.


Mungu ndiye aliyeifanya milima, na kuumba upepo; ndiye anayemujulisha mwanadamu mawazo yake; ndiye anayegeuza muchana kuwa usiku, na kukanyaga vilele vya dunia. Yawe wa majeshi ndilo jina lake!


Mulibeba kama vile sasa sanamu za mungu wenu Sakuti mufalme wenu na sanamu za Kiuni mungu wenu wa nyota, vitu ambavyo mulijitengenezea wenyewe?


Ole kwenu ninyi munaostarehe kule Sayuni, nanyi munaoishi katika usalama kwenye mulima Samaria! Ninyi munaonekana kuwa waongozi wa taifa kubwa, ambao Waisraeli wote wanawategemea.


Kwa hiyo mutakuwa wa kwanza kwenda katika uhamisho, na karamu za wenye kustarehe zitatoweka.


Mulitembea mukibeba hema ya mungu wenu Moleki nayo sanamu ya nyota ya mungu wenu Refani. Mulijitengenezea sanamu hizo kusudi muziabudu. Kwa hiyo nitawahamisha mbali kupita muji Babeli.’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ