Nilifanya hivyo kwa sababu waliyakataa maagizo yangu, hawakufuata masharti yangu, wakazikufuru Sabato zangu; maana walijitoa kwa moyo juu ya sanamu za miungu yao.
Lakini waliniasi, hawakutaka kunisikiliza. Hakuna hata mumoja kati yao aliyetupilia mbali machukizo yale waliyoyapenda, wala hawakuachana na sanamu za miungu ya Misri. Basi, nikafikiri kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuitimiza hasira yangu juu yao wakiwa kulekule katika inchi ya Misri.
Kwa hiyo Waisraeli watakoma kabisa kuwatambikia miungu ya uongo wenye umbo la beberu, jambo ambalo limewafanya wakose uaminifu kwangu. Hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyao vyote.
Uwaambie wakaaji wote wa inchi na makuhani hivi: Kwa muda wa miaka makumi saba iliyopita, ninyi mulikuwa mukifunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba. Munazani mulifunga kwa ajili yangu?
“Sasa, basi, mumutii Yawe na kumutumikia kwa moyo wa haki na uaminifu. Muache kabisa miungu ile ambayo wazee wenu waliiabudu ngambo ya muto Furati na katika inchi ya Misri. Mumutumikie Yawe.