Amosi 5:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
15 Muchukie mabaya, mupende mazuri, na kudumisha sheria ya Mungu katika tribinali. Labda Yawe wa majeshi atawarehemu watu wa kabila la Yosefu waliobaki.
Watumishi wake wakamwendea, wakamwambia: “Tumesikia kwamba wafalme wa Israeli ni wema. Basi, uturuhusu tujifunge magunia kwenye viuno na kamba katika shingo, tumwendee mufalme wa Israeli. Labda atayaokoa maisha yako.”
Yoahazi hakukuwa na waaskari, lakini alikuwa tu na wapanda-farasi makumi tano, magari kumi na waaskari wa miguu elfu kumi. Hii ilikuwa ni kwa sababu mufalme wa Aramu alikuwa ameyaangamiza makundi ya waaskari ya Israeli na kuyakanyaga chini kama mavumbi.
Wakati wa utawala wa Peka mufalme wa Israeli, Tigilati-Pileseri, mufalme wa Asuria, aliteka miji ya Iyoni, Abeli-Beti-Maka, Yanoa, Kadesi na Hazori, pamoja na inchi za Gileadi, Galilaya na Nafutali na kuwahamisha wakaaji wake kwenda Asuria.
Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyosikia. Uwaombee watu wanaobaki.’ ”
Yawe anasema hivi: Mufuate sheria yangu na kutenda kwa haki. Muokoe kila mutu aliyenyanganywa mali zake toka katika mikono ya mutesaji. Musiwatendee vibaya au kwa ukali wageni, wayatima na wajane, wala musimwange damu ya mutu asiyekuwa na kosa kwa nafasi hii.
Maana Yawe anasema hivi: Mushangilie kwa furaha kwa ajili ya Yakobo, mupige vigelegele kwa ajili ya taifa kubwa, mutangaze, musifu na kusema: Yawe ameokoa watu wake, ameleta ukombozi kwa wale waliobaki kati ya Waisraeli!
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninyi wakubwa wa Waisraeli, mumefanya zambi vyakutosha. Muache kutesa watu kwa ukali. Muimarishe sheria yangu na haki. Muache kuwafukuza watu wangu katika inchi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
Danieli akamwomba mufalme, naye mufalme akawaweka Sadiraki, Mesaki na Abedenego kuwa wasimamizi wa mambo ya utawala ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli akabakia katika nyumba ya mufalme.
Mutafute Yawe, nanyi mutaishi! Kama sivyo, atawatokea wazao wa Yosefu kama moto; moto utawateketeza wakaaji wa Beteli na hakuna mutu atakayeweza kuuzimisha.
Farasi wanaweza kukimbia katika mawe makubwa? Watu wanaweza kulima bahari na ngombe? Lakini ninyi mumeigeuza sheria kuwa sumu, na tunda la haki kuwa uchungu.
Kapiteni wa mashua akamwendea, akamwambia: Namna gani wewe unaweza kulala? Amuka umwombe Mungu wako; labda Mungu wako atatuhurumia na kuyaokoa maisha yetu.
Lakini kweli nitawakusanya ninyi wote enyi watu wa Yakobo, nitawakusanya enyi Waisraeli muliobaki, niwalete pamoja kama kondoo katika zizi, kama kundi kubwa la kondoo katika shamba la malisho; nanyi mutakuwa kundi la watu wengi.
Huyo mutawala atawachunga watu wake kwa nguvu ya Yawe, kwa utukufu wa Yawe, Mungu wake. Watu wake wataishi kwa usalama, maana atakuwa mukubwa mpaka kwa miisho ya dunia.
Mutafute Yawe, enyi wanyenyekevu wote katika inchi, enyi munaozitii amri zake. Mutafute haki, mutafute unyenyekevu; labda mutaiponyoka siku ya kasirani ya Yawe.
Mupendwa wangu, usifuate mufano mubaya, lakini ufuate mufano muzuri. Mutu anayetenda mema ni mutoto wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hashirikiani na Mungu.