Amosi 5:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Maana mimi ninajua wingi wa makosa yenu na ukubwa wa zambi zenu; ninyi munawatesa watu wema, munapokea kituliro na kuzuia wakosefu wasipate haki katika tribinali.
Wakubwa wako ni waasi; wanashirikiana na wizi. Kila mumoja anapenda kituliro, na kukimbilia zawadi. Hawamupatii yatima haki yake, haki za wajane si kitu kwao.
Ni mutu anayekuwa hivi: anaishi kwa haki na kusema kwa usawa, anazarau kabisa utajiri wa unyanganyi, anakataa kupokea kituliro, hakubali hata kidogo kusikia mipango ya mauaji, wala hakubali macho yake yaone maovu.
Haya yote mawili yatakupata kwa rafla katika siku moja: kupoteza watoto wako na kuwa mujane, ijapokuwa una wingi wa uchawi wako, na nguvu nyingi za uganga wako.
Jambo hili litawafikia kwa sababu wametenda katika Israeli mambo yasiyofanyika. Walizini na wake za jirani zao, na kusema maneno ya uongo kwa jina langu, jambo ambalo mimi sikuwaamuru wafanye. Mimi ninajua hayo. Nimeyashuhudia. –Ni ujumbe wa Yawe.
Kwa sababu mumewavunja watu wa haki moyo kwa kusema uongo, ijapokuwa mimi sikuwavunja moyo, mukawaimarisha waovu wasiache mienendo yao mibaya na kuokoa maisha yao,
Waamuzi wanahukumu kwa kupewa kutuliro, makuhani wake wanafundisha kwa kupata malipo, manabii wanatabiri kwa kupata feza. Hata hivyo wanajidai kumutegemea Yawe, wakisema: Yawe, si yupo pamoja nasi? Hatutapatwa na hasara yoyote!
Wote ni wafundi wa kutenda maovu; waongozi na waamuzi wanaomba kituliro. Wakubwa wanaonyesha wazi nia zao mbaya, nao wanashirikiana pamoja kwa kuzitimiza.
Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.
Ni nani kati ya manabii ambaye babu zenu walikosa kumutesa? Waliwaua wale waliotabiri zamani habari za kuja kwa Mwenye Haki. Na sasa mumemutoa na kumwua.
Watakapopatwa na hasara nyingi na taabu, wimbo huu utakuwa kama ushuhuda maana hautasahauliwa na wazao wao. Hata sasa, mbele sijawapeleka katika inchi niliyoapa kuwapa, ninajua mipango ambayo wanapanga.”
Ninyi hamukulipa mishahara ya watumishi waliotumika katika mashamba yenu. Musikilize mashitaki yao! Malalamiko ya wavunaji yamefika katika masikio ya Bwana Mwenye Uwezo!
Boazi akakwenda kwa nafasi ya kufanyia mukutano kule kwenye mulango wa muji, akaikaa chini. Kisha yule ndugu ya Elimeleki ambaye Boazi alikuwa amemutaja, akapita karibu na pale. Boazi akamwita, akasema: “Kuja, uikae hapa ndugu.” Basi yule mutu akakuja na kuikaa pale.