Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 5:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Musikilize maombolezo yangu juu yenu, enyi Waisraeli:

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 5:1
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yawe anasema hivi: Muulize habari kwa mataifa yote: Nani amekwisha kusikia jambo kama hili? Kitendo Waisraeli walichokifanya ni cha kuchukiza sana.


Munyoe nywele zenu na kuzitupa, enyi wakaaji wa Yerusalema: mufanye maombolezo juu ya vichwa vya milima, maana, mimi Yawe nimewakataa ninyi, nimewatupilia ninyi kizazi kilichosababisha hasira yangu!


Yawe anasema: Nitaifanya Yerusalema kuwa mabomoko matupu, nitaifanya kuwa pango la mbweha; na miji ya Yuda nitaifanya kuwa jangwa, pahali pasipokaliwa na mutu yeyote.


Muwaambie hivi: Mukuje upesi muomboleze juu yetu, macho yetu yapate kutiririka machozi, na kope zetu zibubujike machozi kama maji.


Kifo kimetuingilia katika madirisha yetu, kimetupangia katika nyumba zetu nzuri; kimewaangukia watoto wetu katika barabara, nao vijana wetu katika viwanja vya makutano.


Nitalia na kuomboleza juu ya milima; nitaomboleza juu ya mashamba ya nyama katika jangwa, kwa sababu yamekauka kabisa, hakuna mutu anayepita pahali pale. Hakusikiliki tena sauti za ngombe; ndege na nyama wamekimbia na kutoweka.


Mungu aliniambia niimbe wimbo huu wa maombolezo juu ya wakubwa wa Waisraeli:


Lakini moto umetoka kwenye shina lake, ukayateketeza matawi na matunda yake. Matawi yake hayatakuwa na nguvu hata kidogo, wala hayatakuwa fimbo za kifalme. Huo umekuwa wimbo wa maombolezo; ndivyo unavyoimbwa siku zote.


Watakuimbia wimbo huu wa kuomboleza: Namna gani wewe muji wenye utukufu, umetoweka kutoka katika bahari! Ulikuwa na nguvu juu ya bahari, wewe pamoja na wakaaji wako, wewe uliyeletea woga juu ya wote!


Sasa ewe mwanadamu, imba wimbo huu wa maombolezo juu ya muji wa Tiro.


Wewe mwanadamu! Imba wimbo wa maombolezo juu ya mufalme wa Tiro. Umwambie kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wewe mufalme wa Tiro ulikuwa mupaka wa ukamilifu; ulijaa hekima na uzuri kamili.


Huo ndio wimbo wa maombolezo, wanawake wa mataifa watauimba, wataimba juu ya Misri na watu wake wote. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Wewe mwanadamu! Imba wimbo wa kuomboleza juu ya Mufalme wa Misri. Wewe Mufalme wa Misri unajiona kuwa simba kati ya mataifa, lakini wewe ni kama mamba tu katika maji: unachomoka kwa nguvu kwenye mito yako, unayavuruga maji kwa miguu yako, na kuichafua mito.


Enyi Waisraeli, musikilize neno Yawe alilosema juu yenu, enyi taifa zima alilolitoa katika inchi ya Misri:


Musikilize neno hili, enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria. Ninyi munaowaonea wamasikini, munaowagandamiza wakosefu, na kuwaambia waume zenu: Mutuletee divai tukunywe! Musikilize ujumbe huu:


Basi, Yawe, Mungu wa majeshi, Bwana wetu anasema hivi: Kutakuwa kilio kila nafasi katika barabara za muji; watu wataomboleza: Ole! Ole! Walimaji wataitwa kuja kuomboleza, na wafundi wa kuomboleza kuja kufanya kilio.


Wale wanaoapa kwa mungu wa uongo wa Samaria na kusema “Kwa nafsi ya mungu wako ee Dani” au “Kwa nafsi ya mungu wa Beri-Seba”, wote wataanguka na hawatasimama tena hata kidogo.


Siku hiyo watu watawasimanga kwa wimbo, watalia na kuomboleza kwa uchungu, wakisema: Tumeangamia kabisa; amekamata inchi yetu, ameiondoa katika mikono yetu. Mashamba yetu ameyagawanya kwa wale waliotuteka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ