Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 4:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Niliwapiga pigo la ukosefu wa maji na ukungu; nikakausha bustani na mashamba yenu ya mizabibu; nzige wakakula miti ya tini na mizeituni yenu. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 4:9
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Ikiwa kuna njaa katika inchi, au ugonjwa mukali, ukosefu wa mvua, ugonjwa wa mimea, nzige au vidudu vingine, au ikiwa watu wako wameshambuliwa na waadui zao katika muji wao wowote, ikiwa kuna pigo lolote au ugonjwa wowote,


“Ikiwa kuna njaa katika inchi au ugonjwa mukali, ukosefu wa mvua, ugonjwa wa mimea, nzige au vidudu vingine, au ikiwa watu wako wakishambuliwa na waadui zao katika muji wao wowote, ikiwa kuna pigo lolote au ugonjwa wowote,


Niwapige wapi tena, ninyi munaoendelea kuasi? Kichwa chote kinajaa vidonda, na moyo unaumia kabisa!


Lakini ninyi munaowasha moto, na kujifanyia silaha za mienge, mutembee kwa mwangaza wa moto huo, ndimi za moto muliowasha ninyi wenyewe. Kitu mutakachopata kutoka kwa Yawe ni hiki: ninyi mutalala chini na mateso makali.


Ingawa aliwaazibu watu, hawakumurudilia Yawe wa majeshi.


Pamoja na hayo yote, Yuda, dada mudanganyifu wa Israeli hakunirudilia kwa moyo wote, lakini kwa unafiki tu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.


Basi, watarudi katika inchi ya Misri; watatawaliwa na mufalme wa Asuria, kwa sababu wamekataa kunirudilia.


Nzige, makundi kwa makundi, wameishambulia mimea; kilichoachwa na nzige kimekuliwa na tunutu, kilichoachwa na tunutu kimekuliwa na parare, kilichoachwa na parare kimeliwa na panzi.


Limeiharibu mizabibu yetu, na kuitafuna mitini yetu. Limeyabandua maganda yake na kuyatupa chini, na matawi yake yameachwa meupe.


Nitawarudishia miaka ile iliyokuliwa na nzige, kila kitu kilichokuliwa na tunutu, parare na panzi, hilo kundi kubwa nililowaletea!


Mimi niliwanyima chochote cha kutafuna, nikasababisha ukosefu wa chakula popote. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Watu wa miji miwili au mitatu wakakimbilia katika muji mwingine, wapate maji, lakini hayakuwatoshelea. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Hata kama miti ya tini isipochanua maua wala mizabibu kuzaa zabibu, hata kama mizeituni isipozaa zeituni na mashamba yasipotoa chakula, hata kama kondoo wakitoweka katika zizi na nyama wa kufugwa kukosekana katika mazizi,


Mimea yenu yote muliyojaribu kupanda, niliiharibu kwa kuikausha na kwa kuipiga kwa ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Wadudu waharibifu nitawazuia wasiyaharibu tena mazao yenu. Mizabibu yenu katika mashamba haitaacha kuzaa matunda.


Yawe atawashambulia kwa kifua kikuu, homa, majipu, joto kali, ukavu, zoruba na ukungu; mambo hayo yatawaandama mpaka muangamie.


Matunda yenu yote na mazao yenu katika mashamba vitashambuliwa na nzige.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ