Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 4:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Watu wa miji miwili au mitatu wakakimbilia katika muji mwingine, wapate maji, lakini hayakuwatoshelea. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 4:8
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ahabu akamwambia Obadia: “Labda tutapata majani na pale tutaokoa farasi na nyumbu wetu wamoja.”


Ingawa aliwaazibu watu, hawakumurudilia Yawe wa majeshi.


Lakini kati ya manabii wa Yerusalema, nimeona mambo ya kutisha zaidi: wao wanafanya uzinzi na kusema uongo; wanawaunga mukono wanaotenda maovu hata kusikuwe mutu anayeachana na uovu. Kwangu wote wamekuwa kama watu wa Sodoma; wakaaji wake wamekuwa kama watu wa Gomora.


Ndiyo maana manyunyu yamezuizwa kuanguka, wala mvua za mwisho hazijanyesha. Hata hivyo unakausha macho kama kahaba, wala hauna haya hata kidogo.


Mimi nilizani kwamba nyuma ya kufanya hayo yote, atanirudilia. Lakini hakunirudilia. Yuda, dada yake mudanganyifu, alishuhudia hayo yote.


Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.


Basi, watarudi katika inchi ya Misri; watatawaliwa na mufalme wa Asuria, kwa sababu wamekataa kunirudilia.


Kiburi cha Waisraeli kinawashuhudia wao wenyewe, hawanirudilii mimi Yawe, Mungu wao; wala hawanitafuti kwa ajili ya matukio hayo yote.


Mimi niliwanyima chochote cha kutafuna, nikasababisha ukosefu wa chakula popote. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Mutakula lakini hamutashiba; njaa itazidi kuwa katika tumbo yenu. Mukiweka akiba haitachungwa, na mukichunga kitu nitakiharibu kwa vita.


Munapanda mbegu kwa wingi, lakini munavuna kidogo. Munakula, lakini hamushibi. Munakunywa divai, lakini hamutosheki. Munavaa nguo, lakini bado munasikia baridi. Mushahara wa mutumishi unakuwa kama umetumbukizwa katika mufuko uliotoboka.


Mimea yenu yote muliyojaribu kupanda, niliiharibu kwa kuikausha na kwa kuipiga kwa ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ