Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 4:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Mimi niliwanyima chochote cha kutafuna, nikasababisha ukosefu wa chakula popote. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 4:6
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”


Basi, Elia akaenda kujionyesha kwa Ahabu. Wakati huo, njaa ilikuwa kali sana kule Samaria.


Elisha akarudi Gilgali wakati katika inchi kulikuwa njaa. Siku moja, alipokuwa akifundisha wanafunzi wa manabii alimwambia mutumishi wake: “Weka chungu kikubwa juu ya moto, uwapikie manabii chakula.”


Elisha alikuwa amemwambia mwanamuke aliyeishi Sunemu ambaye alikuwa amemufufua mwana wake: “Ondoka na jamaa yako, uhamie katika inchi ya kigeni kwa sababu Yawe ameleta njaa itakayokuwa katika inchi kwa muda wa miaka saba.”


Wakati alipokuwa katika taabu zaidi, mufalme huyu Ahazi alizidi kumwasi Yawe.


Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!


Sasa, Bwana wetu Yawe wa majeshi ataondoa kutoka Yerusalema na inchi ya Yuda kila tegemeo: tegemeo lote la chakula na la kinywaji.


Ingawa aliwaazibu watu, hawakumurudilia Yawe wa majeshi.


Yawe atakata katika Israeli kichwa na mukia, tawi la mingazi na nyasi, kwa muda wa siku moja tu.


Nikienda inje katika mbuga, ninaiona maiti ya waliouawa kwa vita; nikiingia ndani katika muji, ninaona tu maiti ya waliokufa kwa njaa! Manabii na makuhani wanashugulikia mambo yao katika inchi, lakini hawajui wanalofanya.


Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.


Lakini Bwana wetu Yawe anasema: Tena nitauazibu Yerusalema kwa mapigo yangu mane ya hukumu kali: vita, njaa, nyama wakali na ugonjwa mukali, nipate kuangamiza watu na nyama ndani yake!


Basi, niliunyoosha mukono wangu kwa kukuazibu. Nilipunguza chakula chako, nikakuachilia kwa waadui zako, wabinti za Wafilistini ambao walipata haya sana juu ya tabia yako chafu sana.


Basi, watarudi katika inchi ya Misri; watatawaliwa na mufalme wa Asuria, kwa sababu wamekataa kunirudilia.


Nitarudi mahali pangu na kujitenga nao mpaka watambue kosa lao na kunirudilia. Taabu zao zitawafundisha wanitafute.


Mazao yetu yameharibiwa mbele ya macho yetu. Furaha na kicheko vimetoweka katika nyumba ya Mungu wetu.


Kama hata kisha azabu hiyo bado hamunigeukii mimi, lakini munazidi kupingana nami,


Chakula chenu nitakipunguza hata wanawake kumi watumie mafika moja tu kwa kupika mikate. Watawagawanyia mukate wenu kwa kipimo. Na hata kisha kula mutaendelea kuwa na njaa tu.


Mimea yenu yote muliyojaribu kupanda, niliiharibu kwa kuikausha na kwa kuipiga kwa ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Mutapanda mbegu nyingi lakini mutavuna kidogo tu kwa sababu nzige watakula mazao yenu.


Nimemwachia wakati wa kugeuka toka zambi zake, lakini hataki kuacha uasherati wake.


Hapo zamani, wakati waamuzi walipokuwa wanatawala Waisraeli, kulitokea njaa katika inchi. Mutu mumoja kutoka Betelehemu katika Yuda pamoja na muke wake na watoto wao wanaume wawili walikwenda kuishi kwa muda katika inchi ya Moabu kwa kuishi kama wageni.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ