Basi, sehemu ya ukuta wa muji ukabomolewa, naye mufalme pamoja na waaskari wote wakakimbia wakati wa usiku wakipitia katika bustani ya mufalme kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakaenda upande wa Araba, ingawa Wababeli walikuwa wameuzunguka muji.
Watu hao wakaenda mpaka Yordani na katika njia waliona nguo na vifaa vingine Waaramu walivyoacha walipokuwa wanakimbia. Wakarudi na kumupasha mufalme habari.
Basi, sehemu ya ukuta wa muji ilibomolewa na waaskari walikimbia. Wakatoka inje ya muji wakati wa usiku wakipitia njia ya mulango katikati ya kuta mbili, kwenye bustani ya mufalme, ingawa Wakaldea walikuwa wameuzunguka muji wote. Wakakimbia kuelekea bonde la muto Yordani.
Naye mutawala wao atabeba muzigo wake juu ya mabega wakati wa usiku, atatoka kupitia ukuta atakaotoboa apate kutoka; atafunika uso wake kusudi asiione inchi kwa macho yake.
Feza yao wala zahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe. Kwa moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa. Kwa ukamilifu na kwa namna ya kuogopesha atawafanya wakaaji wote katika dunia watoweke.
Kabila la Gileadi lilibaki ngambo ya Yordani. Kabila la Dani, kwa nini mulibaki ndani ya mashua? Kabila la Aseri lilitulia kule pembeni ya bahari, lilikaa katika kivuko chake.