Kwa vile umefanya mipango juu yangu na nimesikia majivuno yako, nitatia ndoana yangu ndani ya pua yako, na lijamu yangu ndani ya kinywa chako. Nitakurudisha katika njia ileile uliyokuja ndani yake.
Nitaita wavuvi wengi kuja kuwanasa watu hawa. Kisha, nitaita wawindaji wengi kuja kuwawinda juu ya kila mulima, kila kilima na katika mapango ya chini ya mawe.
Nitawatafuta kondoo waliopotea na waliotangatanga nitawarudisha kwa nyumba. Waliovunjika nitawatunza, na wale wanaokuwa zaifu nitawapatia nguvu. Lakini kondoo wanono na wenye nguvu nitawaangamiza. Mimi nitawachunga kondoo kama inavyostahili.
Mimi nitakugeuza na kukutia ndoana katika mataya yako, na kukutoa inje wewe pamoja na kundi lako lote la waaskari: farasi na waaskari wapanda-farasi na kundi kubwa la watu wanaovaa nguo za vita, ngao kubwa na ndogo katika mikono pamoja na mapanga yao.
Bwana wetu Yawe ameapa kwa nafsi yake: Ninachukizwa sana na kiburi cha wazao wa Yakobo; tena ninachukia nyumba zao nzuri sana. –Ni ujumbe wa Yawe.– Muji wao na vyote vinavyokuwa ndani yake nitavipatia waadui zake.