Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Bwana wetu Yawe Mutakatifu ameapa: Siku zinakuja ambapo watu watawakokota kwa ndoana kubwa, kila mumoja wenu kama samaki kwenye ndoana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 4:2
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sitavunja agano langu naye, wala kugeuza neno nililosema kwa mudomo wangu.


“Nimeapa mara moja tu kwa utakatifu wangu; nami sitamwambia Daudi uongo.


Kwa vile umefanya mipango juu yangu na nimesikia majivuno yako, nitatia ndoana yangu ndani ya pua yako, na lijamu yangu ndani ya kinywa chako. Nitakurudisha katika njia ileile uliyokuja ndani yake.


Nitaita wavuvi wengi kuja kuwanasa watu hawa. Kisha, nitaita wawindaji wengi kuja kuwawinda juu ya kila mulima, kila kilima na katika mapango ya chini ya mawe.


Basi, nitakutia ndoana katika mataya yako, na kuamuru samaki wakwame katika magamba yako. Nitakuvua kutoka huko ndani ya muto.


Nitawatafuta kondoo waliopotea na waliotangatanga nitawarudisha kwa nyumba. Waliovunjika nitawatunza, na wale wanaokuwa zaifu nitawapatia nguvu. Lakini kondoo wanono na wenye nguvu nitawaangamiza. Mimi nitawachunga kondoo kama inavyostahili.


Mimi nitakugeuza na kukutia ndoana katika mataya yako, na kukutoa inje wewe pamoja na kundi lako lote la waaskari: farasi na waaskari wapanda-farasi na kundi kubwa la watu wanaovaa nguo za vita, ngao kubwa na ndogo katika mikono pamoja na mapanga yao.


Bwana wetu Yawe ameapa kwa nafsi yake: Ninachukizwa sana na kiburi cha wazao wa Yakobo; tena ninachukia nyumba zao nzuri sana. –Ni ujumbe wa Yawe.– Muji wao na vyote vinavyokuwa ndani yake nitavipatia waadui zake.


Yawe, utukufu wa Yakobo, ameapa: Hakika, sitayasahau matendo yao maovu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ