Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 4:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Mungu ndiye aliyeifanya milima, na kuumba upepo; ndiye anayemujulisha mwanadamu mawazo yake; ndiye anayegeuza muchana kuwa usiku, na kukanyaga vilele vya dunia. Yawe wa majeshi ndilo jina lake!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 4:13
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Anaamuru jua lisipande, anafunika nyota zisiangaze.


Analeta mawingu kutoka miisho ya dunia, anapiga umeme na kunyesha mvua, anavumisha upepo kutoka gala zake.


Nikiikaa au nikisimama, wewe unajua; wewe unajua kila kitu ninachofikiri juu yake.


Anapoamuru, hayo mawe yanayeyuka; anapovumisha upepo, maji yanatiririka.


Kwa matendo yako makubwa unatuitikia na kutuokoa, ewe Mungu mwokozi wetu. Wewe ndiwe tumaini la viumbe vyote katika dunia yote na mbali katika bahari.


Basi, Musa akanyoosha mukono wake juu mbinguni, kukakuwa giza nzito katika inchi yote ya Misri kwa muda wa siku tatu.


Ukakaa katikati ya Waisraeli na Wamisri. Lile wingu likawatia Wamisri giza, lakini likawaangazia Waisraeli usiku. Kwa hiyo, makundi hayo mawili, jeshi la mufalme wa Misri na kundi la Waisraeli, hayakukaribiana usiku kucha.


Ni nani anayeweza kupima maji ya bahari katika kitanga cha mukono wake, na kuzipima mbingu kwa mikono yake? Ni nani anayeweza kuutia udongo wa dunia katika kikombe; kuipima milima kwa mizani au vilima kwa kipimo cha uzito?


Mimi ninafanya mwangaza na kuumba giza; ninaleta uheri na kusababisha hasara. Mimi Yawe ninatenda vitu hivi vyote.


Mukombozi wetu ndiye Mutakatifu wa Israeli; Yawe wa majeshi ndilo jina lake.


Ninyi munaona utukufu kujiita watu wa muji mutakatifu, na kujidai kumutegemea Mungu wa Israeli, ambaye jina lake ni Yawe wa majeshi.


Siku hiyo, watanguruma juu ya Israeli kama uvumi wa bahari iliyochafuka. Atakayeiangalia inchi kavu ataona giza tupu na taabu, mwangaza utafunikwa na mawingu.


Anapotoa sauti, maji yananguruma katika mbingu, anapandisha mawingu toka kwa miisho ya dunia. Anaufanya umeme upige wakati wa mvua, na kuuvumisha upepo katika gala zake.


Lakini Mungu wa Yakobo si kama sanamu hizo, maana, yeye ndiye aliyeumba vitu vyote, na Israeli ni taifa linalokuwa mali yake; Yawe wa majeshi, ndilo jina lake.


Mumutukuze Yawe, Mungu wenu, mbele hajawaletea giza, mbele hamujajikwaa miguu kwenye milima inayofunikwa na giza. Ninyi mulitazamia mwangaza, lakini anaugeuza kuwa usiku anaufanya kuwa giza nzito.


Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa mufalme, jina lake Yawe wa majeshi– kweli adui anakuja kuwashambulia: ni hakika kama vile Tabori unavyokuwa mulima, kama vile mulima Karmeli unavyoonekana kutoka katika bahari.


Anapotoa sauti yake maji yanajikusanya mbinguni, anafanya ukungu upande kutoka mipaka ya dunia. Anafanya umeme upige wakati wa mvua, anavumisha upepo kutoka gala zake.


Mungu anayekuwa hazina ya Yakobo si kama hizo, maana yeye ndiye aliyeviumba vitu vyote, na Israeli ni kabila linalokuwa mali yake; Yawe wa majeshi, ndilo jina lake.


Lakini, kuna Mungu mbinguni ambaye anafumbua mafumbo, naye amekujulisha, ee mufalme Nebukadneza, mambo yatakayotukia katika siku zinazokuja. Ndoto yako na maono yaliyokufikia ulipokuwa unalala ni haya:


Lakini mimi sikufumbuliwa fumbo hili kwa sababu nina hekima kuliko wanadamu wengine, lakini kusudi wewe mufalme, upate kujulishwa maana ya ndoto yako na kujua mawazo yako.


Hiyo ni siku ya giza na huzuni; siku ya mawingu na giza nene. Jeshi kubwa linakaribia kama giza linalofunikia milima. Namna hiyo haijapata kuwa hata kidogo wala haitaonekana tena katika vizazi vyote vinavyokuja.


Musikilize, muwaonye wazao wa Yakobo. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe, Mungu wa majeshi.–


Kwa hiyo nitawapeleka katika uhamisho, mbali kuliko Damasiki! –Ni Yawe anayesema, ambaye jina lake ni Mungu wa majeshi.


Huyo aliyezifanya nyota zinazoitwa Kilimia na Orioni, ambaye analigeuza giza nene kuwa muchana, na muchana kuwa usiku; yeye anayekusanya maji ya bahari na kuyamwanga juu ya inchi kavu, Yawe ndilo jina lake.


Bwana wetu Yawe ameapa kwa nafsi yake: Ninachukizwa sana na kiburi cha wazao wa Yakobo; tena ninachukia nyumba zao nzuri sana. –Ni ujumbe wa Yawe.– Muji wao na vyote vinavyokuwa ndani yake nitavipatia waadui zake.


Siku hiyo, nitalifanya jua litue pa saa sita za muchana, na kuijaza inchi giza wakati wa muchana. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Yawe amejenga makao yake mbinguni, nayo dunia akaifunika kwa anga; anayaita maji ya bahari, na kuyamwanga juu ya inchi kavu. Yawe, ndilo jina lake!


Kweli, anakuja kutoka makao yake; atashuka na kutembea juu ya vilele vya dunia.


Bwana, Yawe ndiye nguvu yangu, anaimarisha miguu yangu kama ya paa, ananiwezesha kupita juu katika milima. Kwa mwimbishaji: pamoja na ala za muziki wa nyuzi.


Ujumbe wa Yawe unaoelekea Israeli. Yawe aliyezitandaza mbingu, aliyeiweka misingi ya dunia na kumupa mwanadamu uzima anasema hivi:


Naye Yesu akijua mafikiri yao, akawauliza: “Sababu gani munawaza maneno hayo mabaya?


Naye hakuhitaji kupewa ushuhuda juu ya mutu yeyote, kwa maana yeye mwenyewe alijua yanayokuwa ndani ya mioyo ya watu.


Upepo unavuma pahali unapotaka, nawe unasikia sauti yake, lakini haujui pahali unapotoka wala unapokwenda. Na ni vile inavyokuwa kwa kila mutu anayezaliwa kwa Roho.”


Aliwapitisha katika inchi za juu za vilima, nao wakakula mazao ya mashamba. Akawapa asali kutoka katika mawe waonje na mafuta kutoka katika jiwe gumu.


Heri yenu ninyi Waisraeli. Nani anayekuwa kama ninyi, watu muliookolewa na Yawe, ambaye ndiye ngao ya musaada wenu, na upanga unaowaletea ushindi! Waadui zenu watakuja wananyenyekea mbele yenu, nanyi mutawakanyaga chini.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ