Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Simba akinguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana wetu Yawe akisema, ni nani atakataa kuutangaza ujumbe wake?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 3:8
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ewe Israeli, watu wangu, enyi muliotwangwa na kupepetwa kama ngano. Sasa nimewaambia ninyi mambo niliyoyasikia kwa Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli.


Yawe aliniambia hivi: Simba mukali ananguruma kwa kukinga nyama aliyemukamata; hata kundi la wachungaji likiitwa kwa kumufukuza, hatishiki kwa kelele zao, wala hashituki kwa sauti zao. Ni vile Yawe wa majeshi atakavyoshuka kupigana juu ya mulima Sayuni na kilima chake.


Lakini ninaposema “Sitamutaja tena Yawe, wala sitasema tena kwa jina lake”, ndani yangu kunawaka kitu kama moto uliofungiwa ndani ya mifupa yangu. Ninajaribu sana kuuzuia humo, lakini ninashindwa.


Halafu Yeremia akawaambia wakubwa na watu wote: Yawe alinituma niwatabirie mambo yote muliyosikia nikisema juu ya hekalu hili na muji huu.


Siku hiyo, nitawafanya Waisraeli wakuwe na nguvu na kukuwezesha wewe Ezekieli useme kati yao. Nao watapata kujua kwamba mimi ni Yawe.


Amosi alisema hivi: Yawe ananguruma toka mulima Sayuni, anavumisha sauti yake toka Yerusalema, hata mashamba ya malisho ya wachungaji yanakauka, majani ya mulima Karmeli yananyauka.


Ninyi muliwakunywesha wanaziri divai, na kuwaamuru manabii wasitoe unabii.


Simba ananguruma katika pori kama hajapata nyama? Simba mukali ananguruma katika pango lake kama hajakamata kitu?


Kwa maana sisi hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo tuliyoyaona na kuyasikia.”


“Mwende ndani ya hekalu na mutangaze kwa watu maneno yote yanayoelekea uzima mupya.”


Petro na mitume wengine wakajibu: “Inatupasa sisi kumutii Mungu kuliko watu!


Mimi sina haki ya kujisifu kwa sababu ninatangaza Habari Njema, kwa maana nimelazimishwa kuitangaza. Basi ole kwangu kama nisipotangaza Habari Njema.


Basi mumoja kati ya wale wazee akaniambia: “Usilie. Angalia, simba wa kabila la Yuda, wa uzao wa mufalme Daudi, amepata ushindi. Yeye anaweza kuvunja vile vifundo saba vya muhuri vya kizingo na kukifungua.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ