Nani asiyekuogopa wewe, ee mufalme wa mataifa? Wewe unastahili kuheshimiwa: kwa maana kati ya wenye hekima wote wa mataifa, na katika falme zao zote, hakuna hata mumoja anayekuwa kama wewe.
Uchungu, uchungu! Ninagaagaa kwa uchungu! Moyo wangu unapigapiga vibaya. Wala siwezi kukaa kimya. Maana ninaogopa mulio wa baragumu, ninasikia kelele la vita.
Mutoe tangazo, mupashe habari huko Yerusalema! Mupige baragumu kila pahali katika inchi! Mulalamike, mukisema: Mukusanyike pamoja! Mukimbilie katika miji yenye kuzungukwa na kuta!
Mbona hamuniogopi? –Ni ujumbe wa Yawe.– Kwa nini hamutetemeki mbele yangu? Mimi niliwekea bahari muchanga kuwa mupaka wake; ni kizuizo cha milele ambacho bahari haiwezi kuvuka. Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita; ingawa yanavuma, hayawezi kuuruka.
Enyi watu wa kabila la Benjamina, muondoke Yerusalema, mukimbie! Mupige baragumu katika muji Tekoa! Muonyeshe kitambulisho cha vita huko Beti-Keremu, maana hasara na maangamizi makubwa vinakuja kutoka upande wa kaskazini.
Mbele ya wakati huo, watu hawakupata mushahara kwa kazi zao wala mali kwa ajili ya kutumikisha nyama. Hamukuwa na usalama kwa sababu ya waadui zenu, maana nilisababisha uadui kati ya watu wote.
Mutu huyu alitolewa kwenu kufuatana na mupango uliokusudiwa na kujulikana na Mungu tangu zamani. Nanyi mulimwua, kwa kumutia katika mikono ya wenye zambi wamutundike juu ya musalaba.
Basi, kwa sababu tunajua kwamba ni lazima kumwogopa Bwana, ndiyo maana tunajitoa kuwavuta watu kwake. Mungu anatujua waziwazi nami ninatumaini kwamba ninyi wenyewe munatujua waziwazi vilevile.