Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 3:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Nitaziharibu nyumba zote katika muji na katika vijiji; nitazibomoa nyumba zilizopambwa kwa pembe za tembo, nyumba kubwakubwa zitaanguka. –Ni ujumbe wa Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 3:15
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mambo mengine ya Ahabu, yote aliyofanya, na jinsi alivyojenga na kupamba nyumba yake kwa pembe, na miji yote aliyojenga, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.


Unapenda haki na kuchukia uovu. Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupendelea kuliko wenzako; amekuweka kuwa mufalme kwa kukupakaa mafuta ya kufurahisha.


Nimemusikia Yawe wa majeshi akisema hivi: Hakika nyumba nyingi zitabaki tupu, zile kubwa na nzuri zitabaki wazi bila wakaaji.


Wakati huo ulikuwa mwezi wa kenda, na mufalme alikuwa ndani ya nyumba yake ya nyakati za baridi. Mbele yake kulikuwa moto wa makaa.


Basi, nitashusha moto juu ya inchi ya Yuda, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za Yerusalema.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Waadui wataizunguka inchi yenu, wataharibu kuta zako, na kuziteka nyumba zao nzuri.


Ninyi munawagandamiza wazaifu na kuwalipisha kodi ya ngano. Munajijengea nyumba za mawe ya kuchongwa, lakini ninyi hamutaishi humo; munalima bustani nzuri za mizabibu, lakini hamutakunywa divai yake.


Yawe anatoa amri, na nyumba kubwa inabomoka vipandevipande, na nyumba ndogo kusagikasagika.


Waedomu, wale wazao wa Esau, wanasema kwamba ingawa miji yao imeharibiwa, watajenga upya mabomoko yake. Lakini, Yawe wa majeshi anasema hivi: Wanaweza kuijenga upya, lakini mimi nitaibomoa tena. Watu watawaita: Taifa ovu ambalo Yawe amelikasirikia milele.


Naye Ehudu akamukaribia pale alipokaa katika chumba chake chenye baridi katika baraza, akamwambia: “Nina ujumbe wako kutoka kwa Mungu.” Mufalme akasimama toka juu ya kiti chake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ