Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Amosi 3:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Siku nitakapowaazibu Waisraeli kwa sababu ya makosa yao, nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli. Nitazikata pembe za kila mazabahu na kuziangusha chini.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Amosi 3:14
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Zaidi ya hayo aliharibu kule Beteli pahali pa kuabudia palipojengwa na mufalme Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Aliharibu mazabahu hayo na kuvunja mawe yake vipandevipande, na kisha akaviponda mpaka vikakuwa mavumbi. Vilevile akachoma sanamu ya Ashera.


Nyuma ya sherehe kumalizika, watu wote wa Israeli wakakwenda katika kila muji wa Yuda, wakavunjavunja nguzo za mawe na kukatakata sanamu za Ashera, mungu wa kike, na vilevile wakaharibu mazabahu na pahali pa kuabudia miungu mingine. Wakafanya vile katika inchi yote ya Yuda, Benjamina, Efuraimu na Manase, mpaka walipokwisha kuvimaliza vyote. Kisha Waisraeli wakarudi kwao, kila mutu kwenye urizi wake.


Lakini sasa kwenda uwaongoze watu mpaka pahali nilipokuambia. Malaika wangu atakutangulia. Hata hivyo, siku nitakapowafikia, nitawaazibu kwa sababu ya zambi yao.


Juu ya kila mazabahu, watu wanalalia nguo walizozitwaa kwa masikini kama rehani ya madeni yao; na katika nyumba ya Mungu wao, wanakunywa divai waliyotwaa kwa wenye kuwa na madeni yao.


Enyi Waisraeli, muende basi kule Beteli na kuniasi! Muende Gilgali muongeze makosa yenu! Mutoe sadaka zenu kila asubui na zaka zenu kwa siku ya tatu.


Basi, Amazia kuhani wa muji wa Beteli, akamupelekea mufalme Yeroboamu wa Israeli habari hii: Amosi analeta fitina juu yako katika ufalme wa Israeli. Hotuba zake ni hatari kwa inchi hii.


Usitoe tena unabii hapa katika Beteli, kwa sababu hapa ni pahali ya ibada ya mufalme; ni hekalu la utawala huu.


Kule kwenye vilima ambapo wazao wa Isaka wanatambikia, kutafanywa kuwa uharibifu mutupu na mahekalu ya Waisraeli yatakuwa mabomoko. Nitaushambulia kwa vita ukoo wa mufalme Yeroboamu.


Nilimwona Yawe akisimama pembeni ya mazabahu, naye akaniamuru: Piga zile nguzo za hekalu mpaka misingi yake itikisike. Uvunje zile nguzo ziwaangukie watu juu ya vichwa. Wale watakaobaki nitawaua kwa upanga; hakuna hata mumoja wao atakayeponyoka, hakuna atakayetoroka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ